Posts

Showing posts from August 14, 2017

USHAURI; Hatua Muhimu Za Kuchukua Ili Kuondoka Kwenye Madeni Na Kuongeza Kipato Chako.

Karibu kwenye makala yetu ya leo ya ushauri wa changamoto ambazo zinatuzuia kuwa na maisha ya mafanikio. Changamoto ni nyingi, zipo zinazotokea kutokana na mazingira na pia zipo ambazo tunatengeneza sisi wenyewe, kwa kujua au kutokujua. Kwa vyovyote vile, tunapaswa kutatua changamoto zozote tunazokutana nazo ili kuweza kufanikiwa.  Leo tunakwenda kuangalia changamoto ya madeni na kipato kuwa kidogo. Hivyo tutaangalia ni jinsi gani mtu unaweza kuondoka kwenye madeni na kuweza kuongeza kipato chako ili kuondokana na changamoto za kifedha.  Kabla hatujaingia ndani na kuona hatua za kuchukua, tusome maoni ambayo msomaji mwenzetu ametuandikia;  Nashukuru kwenye makala ya leo uliyoonesha njia ya kuepukana na kujipa presha na wakopaji wasio waaminifu. Umetoa ushauri ambao nimewahi kuutumia, jirani alikopa kwangu sh.20,000/= akaanzisha meza ya nyanya, hajanirudishia pesa hadi sasa lakini ni kweli kuwa sasa haombi kitu kutoka kwangu tena.   Lakini kocha mimi nina tat...

Neymar afunga mechi yake ya kwanza Paris St-Germain

Image
Haki miliki ya pic Neymar alifunga bao mechi yake ya kwanza katika klabu yake mpya ya Paris St-Germain baada ya kununuliwa kwa rekodi ya dunia ya £200m kutokaBarcelona. Raia huyo wa Brazil alichangia katika mabao yote matatu yaliyofungwa na PSG dhidi ya Guingamp ambao wamefanikiwa kudumisha rekodi yao ya kushinda 100% mwanzo wa msimu. Jordan Ikoko alifungua ukurasa wa mabao kwa kujifunga baada ya pasi ya Neymar kwa Edinson Cavani kuzimwa Neymar kisha alimsaidia Cavani kufunga kwa pasi safi kabla ya nyota huyo wa uruguay naye kumpa pasi Neymar ambaye alifunga dakika za mwishomwisho akiwa hatua sita hivi kutoka kwenye lango. Mchezaji huyo wa Brazil mwenye miaka 25 alichezeshwa upande wa kushoto lakini alihusika kati safu ya mashambulizi. Alitamba sana uwanjani kwa kugeresha na kushambulia, ingawa mengi ya makombora yake yalizimwa kabla yake kufanikiwa kufunga dakika za mwisho. Neymar  kwa takwimu Haki miliki ya picha Image caption Neymar aligusa mpira mara 128 - ...

Cristiano Ronaldo apewa kadi nyekundu mechi ya El Clasico

Image
Haki miliki ya pich Image caption Cristiano Ronaldo alikosa mechi nyingi za kujiandaa kwa msimu baada ya kuchezea Ureno Kombe la Mabara Cristiano Ronaldo alifunga bao lakini baadaye akafukuzwa uwanjani huku Real Madrid wakilaza Barcelona 3-1 katika Super Cup ya Uhispania, mechi ya mkondo wa kwanza. Gerard Pique alijifunga kutoka kwa krosi ya Marcelo kabla ya Lionel Messi kusawazisha kupitia mkwaju wa penalti. Ronaldo, aliyeingia kama nguvu mpya alirejesha Real Madrid mbele alipokimbia kutoka katikati ya uwanja na kufunga. Alipewa kadi ya njano kwa kuvua shati lake kusherehekea. Muda mfupi baadaye, alioneshwa kadi nyingine ya manjano kwa kujiangusha na akafukuzwa uwanjani. Marco Asensio alifunga la tatu. Ronaldo aliamini kwamba alifaa kupewa penalti baada yake kuanguka alipokabiliwa na Samuel Umtiti, na alionekana kumsukuma refa baada yake kuoneshwa kadi nyekundu. Ronaldo alikaa dakika 24 pekee uwanjani. Barcelona walionekana kutatizika bila Neymar ambaye alihamia ...