Posts

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KUIFANYA NYUMBA YAKO KUWA BORA NA SALAMA

Image
Habari za siku rafiki, ni tumaini langu kuwa bado unaendelea kuweka juhudi na maarifa kuhakikisha unafikia malengo ambayo umejiwekea mwaka huu. Hilo ni jambo nzuri na hongera kwa kila hatua ambayo umefanikiwa kuifikia. Karibu tena kwenye Makala hii tuendelee kushauriana mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo na uwekezaji wa ardhi na majengo. Katika safari hii wapo baadhi ya marafiki wanapitia changamoto mbalimbali zinazohusiana na uwekezaji huu kutokana na sababu mbalimbali ambazo wengi wao ni kwa sababu ya kukosa maarifa sahihi. Leo nitazungumzia mambo muhimu ya kuzingatia ili kuifanya nyumba yako kuwa bora na salama wakati wote. Hapa nazungumzia uimara wa nyumba kuweza kumudu mazingira kwa muda mrefu pasipo kufanyiwa marekebisho yasiyo na ulazima wowote. Nyumba ni matokeo ya ubunifu na usanifu wa mambo mbalimbali ambayo yanatimiza kiu ya matumizi, ubora na mwonekano uliopo. Ili kuyatimiza haya yafuatayo yanapaswa kuzingatiwa kabla ya ujenzi, wakati wa ujenzi na baada ya ujenzi ili ...

NAIBU SPIKA AFUNGUA MASHIDANO YA MBIO ZA BAISKELI MKOANI SIMIYU

Image
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson (wa pili kushoto) akimkabidhi ufunguo wa pikipiki mshindi wa kwanza kilometa 200 (wanaume), Hamisi Hussein kutoka Arusha katika mashindano ya Baiskeli yaliyofanyika Mjini Bariadi (kulia) ni Mkurugenzi Kampuni ya Jambo Food Products ambayo ni mdhamini, Mhe.Salum Khamis akimpongeza Mshindi huyo Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson (mwenye bendera nyeupe kulia) akifungua mashindano ya Mbio za Baiskeli Mkoa wa Simiyu(Simiyu Jambo Festival) kwa kuruhusu washiri kuanza mashindano hayo Mjini Bariadi. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Tulia Ackson (mwenye baiskeli wa pili kulia) akiwa na viongozi wa Mkoa na baadhi ya Wabunge wa Mkoa wa Simiyu na Viti Maalum kutoka nje ya Mkoa kwa ajili ya kufungua mashindano ya baiskeli yaliyofanyika Mjini Bariadi. Mkurugenzi Kampuni ya Jambo Food Products, Mhe.Salum Hamis ambaye ndio mdhamini wa mashindano ya baiskeli n...

Mwalimu Atiwa Mbaroni kwa Kufanya Mapenzi na Mwanafunzi wake wa Kidato cha Nne

Image
Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Igurubi, Maganga Ngassa  (35) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Igunga kwa tuhuma ya kufanya mapenzi na mwanafunzi wa miaka 17 anayesoma shule ya sekondari kidato cha nne, Kata ya Mwisi wilayani hapa. Mwendesha Mashitaka wa Polisi Igunga, Elimajid Kweyamba alidai mbele ya Hakimu Juhudi Mdonya, kwamba Julai 25, mwaka huu saa 9 alasiri katika nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la Forest au Chacha iliyoko Mtaa wa Mwayunge mjini Igunga, kinyume na sheria za nchi, Ngassa alifanya mapenzi na mwanafunzi  mwenye umri wa miaka 17 anayesoma shule ya sekondari iliyoko Kata ya Mwisi kidato cha nne (jina linahifadhiwa).  Mshitakiwa alikana kutenda kosa hilo ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 18, mwaka huu itakapotajwa tena.

Sifa 10 zilizotajwa na HESLB kwa wanafunzi wanaoomba mikopo

Image
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imetangaza mwongozo na vigezo vya utoaji mikopo na ruzuku kwa mwaka wa masomo 2017/2018 na imeanza kupokea maombi ya mikopo kuanzia tarehe 6 Agosti 2017 hadi tarehe 4 Septemba, 2017. Waombaji wote wa mikopo watarajiwa wanasisitizwa kusoma mwongozo wa utoaji mikopo na ruzuku kwa mwaka wa masomo 2017/2018 pamoja na taratibu nyingine za uombaji mkopo kabla ya kujaza fomu za maombi ya mkopo zinazopatikana kwenye mtandao wa  https://olas.heslb.go.tz Kusoma mwongozo na vigezo vya utoaji mikopo na ruzuku kwa mwaka wa masomo 2017/2018 bofya  hapa   Kusoma hatua za kufuata kufanya maombi ya mkopo na malipo bofya  hapa Hapo chini ni sifa za msingi za mwombaji wa mkopo;

Makonda, Ruge na Tanzania All Stars wanogesha sherehe za uwekaji jiwe la msingi la mradi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga kijijini Chongolieni

Image
 Wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya wanaounda kundi la Tanzania All Stars wakijiandaa kupanda jukwaani kutumbuiza kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016  Wasanii nyota wa filamu wa Bongo Movie wakiwa  kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la mafuta ghafi toka Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga katika sherehe zilizofanyika kijiji cha Chongolieni kilicho nje kidogo mwa jiji la Tanga siku ya Jumamosi Agosti 5, 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwaomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda na Mkurugenzi wa Vipindi wa Clouds FM Bw. Ruge Mutahaba wamalize tofauti zao na kuweka maslahi ya nchi mbele wakati alipohutubia kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa b...