Posts

MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEPTEMBA 26,2017

Image

Nyalandu Alivyojitoa Muhanga Sakata la Tundu Lissu

Image
Mbunge wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu amesema kitendo cha Tundu Lissu kusalimika kifo kwenye tukio la kupigwa risasi ni Mungu tu ndiye aliandika, lakini kinamuumiza zaidi huku akilaumu ameikosea nini nchi mpaka kufanyiwa hivyo. Kupigwa risasi kwa Lissu, ambaye alikuwa Dodoma kutekeleza majukumu yake ya kibunge, kuliwaibua wabunge walioliomba Bunge kuunda timu ya kwenda jijini Nairobi kumjulia hali mwenzao, lakini kiti cha spika kilikataa hoja hiyo kwa maelezo kuwa tayari baadhi yao walishaenda kuwawakilisha. Wabunge ambao wakati huo walikuwa Nairobi ni Freeman Mbowe, ambaye ni mwenyekiti wa Chadema na mbunge wa Hai, na Mchjungaji Peter Msigwa, ambaye ni mbunge wa Iringa Mjini wa chama hicho. Wakati wabunge wakilalamika kukosa ruhusa ya Bunge, kulikuwa na malumbano kuhusu ushiriki duni wa Serikali na Bunge katika kumuuguza Lissu aliyepigwa risasi katika kipindi ambacho alishatoa malalamiko kuwa kulikuwa na watu asiowafahamu waliokuwa wanamfuatilia. Laki...

Ashleigh Amzamisha konta- Wuhan

Image
Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Johanna Konta ameshindwa kufurukuta dhidi ya Ashleigh Barty Mwingereza Johanna Konta ameshindwa kufurukuta dhidi ya Ashleigh Barty baada ya kufungwa katika mchezo wa raundi ya pili katika michuano ya Wazi ya Wuhan, China. katika mchezo huo Konta alijitahidi kukabiliana vikali na mpinzani lakini mwishoo alijikuta anapoteza mchezo kwa kufungwa 6-0 4-6 7-6 (7-3) . Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 amepoteza mechi saba za zamani zilizopita tangu kufikia nusu fainali za Wimbledon. Naye Peng Shuai wa china amemgalagaza Petra Kvitova wa Jamhuri ya Czech seti 7-6 (9-7) 6-7 (5-7) 7-6 (7-3) katika mchezo ambao ulijaa upinzani .

Chelsea kuivaa Atletico Madrid-Klabu Bingwa Ulaya

Image
Image caption UEFA Michuano ya klabu bingwa Ulaya hatua ya makundi inapigwa hii leo jumanne usiku kwa michezo mbalimbali . Kundi E - Sevila inacheza na Maribor, Spartak Moscow dhidi ya Liverpool, Kundi F - Manchester city inacheza na Shakhtar Donetsk, Napoli inacheza na Feyenoord. Kundi G- Besiktas inacheza na Rasen Ballsport , Monaco dhidi ya FC Porto. Kundi H - Apoel Nicosia dhidi ya Tottenham na Borussia Dortmund inachuana na Real Madrid. Kesho Jumatano Kundi A - FC Basel itacheza na Benfica, CSKA Moscow na Manchester United. Kundi- B Anderlecht dhidi ya Celtic, PSG itakwaruzana na Bayern Munich. Kundi C- Qarabag dhidi ya As Roma, Atletico Madrid wanakutana na Chelsea, Kundi - D Juventus itacheza na Olympiacos huku Sporting ikichuana na Barcelona.

Alexander Lacazette Shujaa wa Arsenal

Image
Image caption Mshambuliaji mpya wa klabu ya Arsenal Alexandre Lacazette Mshambuliaji mpya wa klabu ya Arsenal Alexandre Lacazette jana jumatatu usiku alifanikiwa kuifungia mabao 2 - 0 dhidi ya West Bromwich Albion katika mchezo wa Ligi kuu ya England , kwa bao la dakika ya 20 kipindi cha kwanza na bao lingine la dakika ya 67 kipindi cha alilofunga kwa njia ya penati. Alexandre Lacazzete mpaka sasa amevunja rekodi ya Brian Marwood iliyowekwa mwaka 1988 ya kufunga katika michezo mitatu ya mwanzo ya ligi ya Epl. Kwa matokeo hayo yanawafanya Arsenal kubaki katika nafasi ya saba ya msimamo wa ligi kuu Uingereza wakiwa na alama zao 10 huku Manchester City wakiwa kileleni.

Washauri wa Trump wadaiwa kutumia barua pepe binafsi

Image
Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Binti wa Rais Trump, Ivanka ni miongoni mwa washauri wa karibu wa Trump Gazeti moja la Marekani limeandika kuwa, washauri sita wa karibu wa rais Trump wamekuwa wakitumia barua pepe binafsi kuzungumzia masuala yahusuyo Ikulu ya Marekani tangu rais Trump kuingia madarakani. Gazeti la New York times limeyataja majina ya washauri hao na mtoto wake Ivanka ni miongoni mwao. Huku jalada la "Newsweek"lenyewe limeandika kuwa barua pepe alizokuwa anazitumia Ivanka alikuwa anatafuta ushirikiano na makampuni ya kibiashara na aliwatumia nakala wakuu wawili wa ofisi. Wakati wa kampeni za uchaguzi, rais Trump alitishia kuwafunga wapinzani wake pale ambapo Hillary Clinton alipotumia barua pepe yake ya binafsi wakati alipokuwa katibu wa serikali ya Marekani. Na siku ya jumapili, mume wa Ivanka, Jared Kushner alitajwa pia kutumia barua pepe yake binafsi kuwasilisha shughuli za serikali. Gazeti moja la Marekani limeandika kuwa, wa...

Marekani yailalamikia Korea Kaskazini

Image
Image caption Korea Kaskazini walaumiwa Marekani imeilalamikia Korea Kaskazini, kwa kauli yake kuwa ina haki ya kuzitungua ndege za kivita za Marekani hata kama zipo nje ya anga la taifa hilo.  Msemaji wa ikulu ya Marekani ya white house Sarah Huckabee Sanders, amewaambia waandishi wa habari kuwa kauli iliyotolewa na Waziri wa mambo ya kigeni wa Korea Kaskazini kwamba Marekani imetangaza vita,ni ya kipuuzi. Kauli hiyo ya waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini ni kufuatia ujumbe wa Rais Trump kupitia ukurasa wake wa twitter,uliokuwa ukisema utawala wa Pyongyoung hauwezi kudumu kwa muda mrefu. Akizungumza katika kituo cha mafunzo cha kimataifa mjini Washington,Waziri wa mambo ya nje wa Korea Kusini Kang Kyung-wha, amesema dunia inapaswa kupatiwa nafuu na maudhi ya Korea Kaskazini. "Hakika, hii inaonyesha kuwa Korea kaskazini itaendeleza maudhi yake, na katika mazingira kama haya,sisi Korea Kusini na umoja wa mataifa tunapaswa kulishughulikia suala hili kwa umakini m...