Iringaland.blogspot.com ni blog inayohusu vivutio na matukio mbalimbali yanayotokea duniani na Masuala ya Afya kwa ujumla na pia kuna vivutio vingi zikiwepo sehemu za historia mbuga za wanyama misitu mikubwa,sehemu za historia nyingi na mengine mengi yanapatikana kwenye blog hii.wote mnakaribishwa kutangaza kupitia kurasa yetu ya iringaland.blogspot.com na Email:lufumbe@gmail.com Instagram @lufumbe
Gereza la Guantanamo lakaribia kufungwa
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Gereza la Guantanamo lakaribia kufungwa
gereza la Guantanamo linamilikiwa na Marekani
Ikulu
ya White house imesema kuwa mipango ya kulifunga gereza la Guantanamo
Bay nchini Cuba imefikia awamu za mwisho. Rais Barack Obama anasemekana
kupatia kipa umbele suala la gereza hilo tangu aingie madarakani mwaka
wa 2009 lakini limekumbwa na vizuizi kadhaa.
gereza lililo n aulinzi mkali la Guantanamo
Gereza hilo la Guantanamo,
ambalo limepewa jina la umaarufu kuwa Gitmo - limekuwa likitumiwa na
Marekani kuwazuilia wapiganaji kutoka vita vya Iraq na vya Afghanistan
bila kufunguliwa mashtaka yoyote. Rais Obama alitoa agizo la kirais
kufungwa kwa kituo hicho mara moja katika siku yake ya kwanza. Lakini
baraza la Congress lilikataa kuwahamisha wafungwa wa huko kuwaleta
nchini Marekani kutokana na hofu za kiusalama. gereza la Guantanamo
Baadhi ya wadadisi wanaamini
kuwa Marekani ilifungua gereza hilo nje ya ardhi ya Marekani ili
wanajeshi wake wapate fursa ya kutumia mbinu zilizopigwa marufuku katika
ardhi yao za kuwahoji wafungwa.
Gereza hilo pia limekumbwa kwa
miaka mingi na madai ya ukiukajji wa haki za binadamu, ambapo njia
zilizotumika kuwahoji wafungwa zimekashifiwa kuwa ukiukaji mkubwa wa
haki za binadamu. Aidha wafungwa wengi wamedai kuteswa, kupigwa na hata
kulazimishwa kukiri baadhi ya mashtaka. wafungwa katika gereza la Guantanamo wamedai kuteswa
Wafungwa kadhaa maejaribu
kujitoa uhai kutokana na mateso wanayodai kupata huko. Wengine
wamechukua hatua kama kususia kula kwa wiki kadhaa kama njia ya
kulalamika hali duni ya kibinadamu katika gereza hilo. wafungwa kadhaa wamereshwa makwao
Wengi tayari wamerejeshwa nchini mwao japo kunao baadhi ambao wanaaminiwa kuwa hatari zaidi na hivyo hawaja achiliwa.
Msemaji
mmoja wa ikulu ya white house ameambia waandishi kuwa mipango ya
kuwasafirisha wafungwa hao kwa njia salama imefikia awamu za mwisho na
itawasilishwa kwa baraza la Congress, lakini hakutoa maelezo zaidi
Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Watu wenye Ulemavu, Anthony Mavunde, (wa pili kulia) akikabidhi Kombe la SportPesa Super Cup kwa Nahodha wa Gor Mahia, Shakava Haron, baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya AFC Leopards katika mchezo wa fainali uliochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. Na Ripota wa Mafoto Blog, Dar Timu ya Gor Mahia ya Kenya imetwaa ubingwa wa kwanza wa mashindano ya SportPesa Super Cup baada ya kuwasambaratisha wapinzani wao, AFC Leopards kwa mabao 3-0 kwenye uwanja wa Uhuru. Uliozikutanisha timu zote za Kenya uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, Gor Mahia imepata nafasi ya kupambana na timu maarufu ya Ligi Kuu ya Uingereza, Everton FC Julai 13 kwenye uwanja wa Taifa jijini. Mshambuliaji wa Gor Mahia na mfungaji wa bao la kwanza kati ya matatu, Muguna Kenneth, akimtoka beki wa AFC Leopards, Abdallah Salim, wakati wa mchezo wa Fainali...
Haki miliki ya picha Image caption Korea Kaskazini tayari imelaani mazoezi hayo ikisema kuwa hatua hiyo ni sawa na kumwaga mafuta kwenye moto. Marekani na Korea Kusini wanafanya mazoezi ya kila mwaka ya jeshi, ambayo mara nyingi huighadhabisha Korea Kaskazini licha ya wito wa kutaka mazoezi hayo yasifanyike. Wiki iliyopita Korea Kaskazini ilionekana kulegeza kamba baada ya kutisha kuwa itarusha makombora kwenda kisiwa cha Marekani cha Guam, lakini tena ikasema kuwa itafuatilia mienendo ya Marekani. Korea Kaskazini tayari imelaani mazoezi hayo ikisema kuwa hatua hiyo ni sawa na kumwaga mafuta kwenye moto. Haki miliki ya picha Image caption Mazoezi hayo hujumuisha ya ardhini , baharini na angani China na Urusi mwezi Julai zilipendekeza kusitishwa mazoezi ya kijeshi ili nayo Korea Kaskazini iache kuyafanyia majaribio makombora. Marekani inasema kuwa mazoezi hayo yatawahusisha wanajeshi 17,500 wa Marekani na yatadumu kwa kipindi cha siku kumi. 'Kifaa' cha Korea K...
MSANII wa filamu nchini, Haji Salum maarufu kama Mboto , amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zinazodai kuwa nguli wa vichekesho katika tasnia ya uigizaji , Amri Athuman maarufu kama King Majuto amefariki dunia. Mboto baada ya kupata taarifa hizi alifunga safari kuelekea mkoani Tanga ambapo ni nyumbani kwa Mzee Majuto na kumkuta hai, na amekanusha uvumi huo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuposti picha inayowaonyesha yeye na Majuto wakiwa nyumbani kwake, na picha hiyo iliambatana na maneno yafuatayo: “ Baada ya kupata taarifa mbaya kuhusu Mzee Majuto nimelazimika kuja kwake Tanga . Ni kweli anaumwa ila anaendelea vizuri na si kama watu walivyozusha kuwa mzee hatunaye. Kwa sasa mzee ni mzima nipo naye Tanga ,” ameandika Mboto . Siku chache zilizopita, gazeti la Ijumaa Wikienda liliripoti taarifa za kuumwa kwa Mzee Majuto...
Comments
Post a Comment