Iringaland.blogspot.com ni blog inayohusu vivutio na matukio mbalimbali yanayotokea duniani na Masuala ya Afya kwa ujumla na pia kuna vivutio vingi zikiwepo sehemu za historia mbuga za wanyama misitu mikubwa,sehemu za historia nyingi na mengine mengi yanapatikana kwenye blog hii.wote mnakaribishwa kutangaza kupitia kurasa yetu ya iringaland.blogspot.com na Email:lufumbe@gmail.com Instagram @lufumbe
EPL: Klabu gani ina wakati mgumu zaidi msimu wa Krismasi?
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Ilichukua siku 87 kucheza mechi 11 za kwanza Ligi ya Premia.
Lakini mechi 11 zinazofuata zitachezwa katika siku 47 pekee.
Kila moja kati ya klabu zilizo kwenye Ligi Kuu itacheza mechi nne wakati wa sikukuu - mechi moja zaidi ya msimu uliopita.
Msimu uliopita, kila klabu ilikuwa na wiki ya kupumzika kabla ya mechi za Boxing Day isipokuwa Everton.
Mwaka huu, Leicester City watacheza mechi nne - kati ya 23 Desemba na 1 Januari - kipindi cha saa 213.
West Ham, nao watacheza mechi zao nne kwa mwendo wa aste aste kiasi, saa 294 na dakika 45.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMsimu huu klabu ya Arsene Wenger ina nafuu zaidi ya klabu nyingine
Hii ni baada ya mechi yao ya Mkesha wa mwaka Mpya dhidi ya Tottenham kuhamishwa hadi 4 Januari kwa sababu za kiusalama.
Hilo limewapa karibu siku tatu za ziada za kupumzika.
Je, mpangilio kwa klabu mbalimbali ukoje?
Pamoja na Arsenal, mabingwa watetezi Chelsea pia wana mpangilio mwema wa mechi.
Watafaidi kutokana na kuhamishwa kwa mechi yao siku ya Mwaka Mpya hadi tarehe 3 Januari.
Viongozi wa ligi Manchester City pia watakuwa na wakati mzuri wa kupumzika kuliko klabu nyingine, ingawa watakuwa wenyeji wa Watford tarehe 2 Januari. Wageni wao hata hivyo watakuwa wamepumzika siku moja zaidi tangu mechi yao itakayotangulia.
Upande ule mwingine wa ligi, Brighton, Burnley na Bournemouth wote watahitajika kucheza emchi zao katika kipindi cha saa 215 - saa 21 chini ya muda wa wastani wa mechi za kipindi hicho ligini ambao ni saa 236.
Manchester United na Newcastle United pia wana mechi zilizofuatana kwa karibu.
Ni klabu mbili pekee - Huddersfield Town na Stoke City - ambazo hazijakuwa na mechi hata moja ambayo imehamishwa tarehe au kusongezwa muda.
Wachezaji watazidiwa?
Wachezaji na mameneja wa klabu zinazocheza Ligi Kuu ya England wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu kuhusu mpangilio wa mechi Desemba.
Januari waka huu, meneja wa Crystal Palace wakati huo Sam Allardyce alikosoa mpangilio huo baada ya timu yake kushindwa nyumbani na Swansea City.
Hata hivyo, kuna ushahidi unaoonyesha kwamba uwezo wa wachezaji huwa hauathiriwi na uchovu kipindi hiki cha mechi nyingi.
Kwa mujibu wa shirika la takwimu za michezo la Opta, kwa kawaida wachezaji huongeza kiwango chao cha uchezaji - kwa umbali wanaosafiri uwanjani na pia mitimko wanayofanya kwenye mechi - kipindi hiki.
Hakuna ushahidi wowote wa kuonyesha kwamba idadi ya magoli yanayofungwa na wachezaji wakati huo hupungua kutokana na uchovu wa wachezaji.
Katika misimu mitatu iliyopita, mechi zinazochezwa Krismasi na Januari huwa na idadi sawa ya magoli kwa wastani kwa kila mechi (2.7) sawa na mechi za nyakati hizo nyingine za msimu.
Makombora ya jumla kwa kila mechi (25.5 majira ya baridi ukilinganisha na 25.8 nyakati hizo nyingine) ukilinganisha na makombora yanayolenga goli kwa kila mechi (8.4 Desemba na Januari ukilinganisha na 8.5) pia hayana tofauti kubwa.
Suala la iwapo wachezaji huathiriwa na kipindi hicho baadaye kwenye msimu ni jambo ambalo limesalia kuwa mjadala.
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp akizungumzia mechi za Krismasi mwaka 2016 alisema: "Kila mtu anashangaa ni kwa nini England huwa haifanikiwi sana na michuano mbalimbali.
"Jiulize klabu nyingine zote (Ulaya) huwa zinafanya nini wakati huo. Huwa na miguu yao kwenye makochi wakitazama mechi za England."
Meneja wa England Gareth Southgate hata hivyo ameuliza iwapo wachezaji wake pengine wanaweza kufaidi kutokana na mapumziko Krismasi.
Si wachezaji na mameneja pekee wanaotatizwa na mechi za kipindi hicho - kuna mashabiki pia
Mashabiki wa Newcastle watasafiri mbali zaidi kwa mechi za Krismasi - takriban maili 964.
Tottenham mashabiki wao nao watasafiri maili 896 - mara tatu zaidi ya umbali wa mashabiki wa Manchester United (maili 288 ) na mara tano zaidi ya mashabiki wa Burnley (maili 160).
Ili iitwe sabuni inatakiwa -Ngumu kuiisha -Yenye povu jingi -Nyeupe VIAMBATA VYA kutengenezea sabuni Mafuta-mawese,mise,wanyana Maji Caustic soda(costiki soda) VIFAA VYA KUTENGENEZEA Ndoo za plastiki lita 20 nne Diaba 1 Mti wa kukorogea Mashine ya kukorogea Box la kugandishia Mhuri wa biashara Mzani wa saa Vibao vya kukatia VIFAA VYA USALAMA Mask Groves Gum boots Goggles (miwani) Overall Ndoo ya maji au mchanga FORMULA mafuta lt1+caustic soda grm135+maji mls350+sodium siligate prm100. KUCHANGANYA pima maji ktk ndoo ya plastic kisa weka caustic soda ktk maji weka kidogokidogo huku ukikoroga mpaka itakapo yeyuka.mchanganyiko huu unaweza kuchemka na kutoa mosh usiogope. acha ipoe kuanzia masaa 8 nazaidi. KUCHANGANYA NA MAFUTA yeyusha mafuta kwa kuyapasha joto kidogo ambapo unaweza kuyashika, tia sangi na mimina kidogo2 kuchanganya michanganyiko huku ukikoroga. mimina kwenye box la kugandishia acha igande tayari kwa kukata.Pia weka sodium siligate
Utengenezaji wa sabuni hii una njia nyingi Hatua ya kwanza Chemsha vipimo 7 vya mafuta ya mawese au mafuta ya shea hadi ifikie hatua ya kimiminika chuja na yaweke kwenye chungu cha mfinyanzi au chombo cha plastiki. Hatua ya pili Pima vipimo 5 vya maji baridi kwenye chombo cha plastiki ongeza kipimo 1cha sodium hydroxide kwa uangalifu mkubwa kwenye maji acha hadi mchanganyiko huo uyeyuke. Subiri mchanganyiko wa sodium hydroxide na mafuta ukaribie kupoa. Hatua ya tatu Taratibu ongeza mchanganyiko wa sodium hydroxide kwenye mawese,huku ukikoroga haraka haraka bila kusitisha ukitumia ubao .hii ni njia nzuri zaidi. Njia ya pili Chemsha mafuta kwenye joto la kadiri ya 55C Changanya maji na sodium hydroxide na uache mchanganyiko huu upoe hadi kufikia joto hilohilo. Baada ya kuandaa mchanyiko wako changanya vimiminika hivyo viwili huku ukikoroga kwanguvu sana kadiri uwezavyo, taratibu sabuni itageuka kuwa laini. Kabla sabuni haijawa ngumu mwaga sabuni ndani ya kasha la mba...
Image caption Mshambuliaji mpya wa klabu ya Arsenal Alexandre Lacazette Mshambuliaji mpya wa klabu ya Arsenal Alexandre Lacazette jana jumatatu usiku alifanikiwa kuifungia mabao 2 - 0 dhidi ya West Bromwich Albion katika mchezo wa Ligi kuu ya England , kwa bao la dakika ya 20 kipindi cha kwanza na bao lingine la dakika ya 67 kipindi cha alilofunga kwa njia ya penati. Alexandre Lacazzete mpaka sasa amevunja rekodi ya Brian Marwood iliyowekwa mwaka 1988 ya kufunga katika michezo mitatu ya mwanzo ya ligi ya Epl. Kwa matokeo hayo yanawafanya Arsenal kubaki katika nafasi ya saba ya msimamo wa ligi kuu Uingereza wakiwa na alama zao 10 huku Manchester City wakiwa kileleni.
Comments
Post a Comment