Iringaland.blogspot.com ni blog inayohusu vivutio na matukio mbalimbali yanayotokea duniani na Masuala ya Afya kwa ujumla na pia kuna vivutio vingi zikiwepo sehemu za historia mbuga za wanyama misitu mikubwa,sehemu za historia nyingi na mengine mengi yanapatikana kwenye blog hii.wote mnakaribishwa kutangaza kupitia kurasa yetu ya iringaland.blogspot.com na Email:lufumbe@gmail.com Instagram @lufumbe
EPL: Klabu gani ina wakati mgumu zaidi msimu wa Krismasi?
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Ilichukua siku 87 kucheza mechi 11 za kwanza Ligi ya Premia.
Lakini mechi 11 zinazofuata zitachezwa katika siku 47 pekee.
Kila moja kati ya klabu zilizo kwenye Ligi Kuu itacheza mechi nne wakati wa sikukuu - mechi moja zaidi ya msimu uliopita.
Msimu uliopita, kila klabu ilikuwa na wiki ya kupumzika kabla ya mechi za Boxing Day isipokuwa Everton.
Mwaka huu, Leicester City watacheza mechi nne - kati ya 23 Desemba na 1 Januari - kipindi cha saa 213.
West Ham, nao watacheza mechi zao nne kwa mwendo wa aste aste kiasi, saa 294 na dakika 45.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionMsimu huu klabu ya Arsene Wenger ina nafuu zaidi ya klabu nyingine
Hii ni baada ya mechi yao ya Mkesha wa mwaka Mpya dhidi ya Tottenham kuhamishwa hadi 4 Januari kwa sababu za kiusalama.
Hilo limewapa karibu siku tatu za ziada za kupumzika.
Je, mpangilio kwa klabu mbalimbali ukoje?
Pamoja na Arsenal, mabingwa watetezi Chelsea pia wana mpangilio mwema wa mechi.
Watafaidi kutokana na kuhamishwa kwa mechi yao siku ya Mwaka Mpya hadi tarehe 3 Januari.
Viongozi wa ligi Manchester City pia watakuwa na wakati mzuri wa kupumzika kuliko klabu nyingine, ingawa watakuwa wenyeji wa Watford tarehe 2 Januari. Wageni wao hata hivyo watakuwa wamepumzika siku moja zaidi tangu mechi yao itakayotangulia.
Upande ule mwingine wa ligi, Brighton, Burnley na Bournemouth wote watahitajika kucheza emchi zao katika kipindi cha saa 215 - saa 21 chini ya muda wa wastani wa mechi za kipindi hicho ligini ambao ni saa 236.
Manchester United na Newcastle United pia wana mechi zilizofuatana kwa karibu.
Ni klabu mbili pekee - Huddersfield Town na Stoke City - ambazo hazijakuwa na mechi hata moja ambayo imehamishwa tarehe au kusongezwa muda.
Wachezaji watazidiwa?
Wachezaji na mameneja wa klabu zinazocheza Ligi Kuu ya England wamekuwa wakilalamika kwa muda mrefu kuhusu mpangilio wa mechi Desemba.
Januari waka huu, meneja wa Crystal Palace wakati huo Sam Allardyce alikosoa mpangilio huo baada ya timu yake kushindwa nyumbani na Swansea City.
Hata hivyo, kuna ushahidi unaoonyesha kwamba uwezo wa wachezaji huwa hauathiriwi na uchovu kipindi hiki cha mechi nyingi.
Kwa mujibu wa shirika la takwimu za michezo la Opta, kwa kawaida wachezaji huongeza kiwango chao cha uchezaji - kwa umbali wanaosafiri uwanjani na pia mitimko wanayofanya kwenye mechi - kipindi hiki.
Hakuna ushahidi wowote wa kuonyesha kwamba idadi ya magoli yanayofungwa na wachezaji wakati huo hupungua kutokana na uchovu wa wachezaji.
Katika misimu mitatu iliyopita, mechi zinazochezwa Krismasi na Januari huwa na idadi sawa ya magoli kwa wastani kwa kila mechi (2.7) sawa na mechi za nyakati hizo nyingine za msimu.
Makombora ya jumla kwa kila mechi (25.5 majira ya baridi ukilinganisha na 25.8 nyakati hizo nyingine) ukilinganisha na makombora yanayolenga goli kwa kila mechi (8.4 Desemba na Januari ukilinganisha na 8.5) pia hayana tofauti kubwa.
Suala la iwapo wachezaji huathiriwa na kipindi hicho baadaye kwenye msimu ni jambo ambalo limesalia kuwa mjadala.
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp akizungumzia mechi za Krismasi mwaka 2016 alisema: "Kila mtu anashangaa ni kwa nini England huwa haifanikiwi sana na michuano mbalimbali.
"Jiulize klabu nyingine zote (Ulaya) huwa zinafanya nini wakati huo. Huwa na miguu yao kwenye makochi wakitazama mechi za England."
Meneja wa England Gareth Southgate hata hivyo ameuliza iwapo wachezaji wake pengine wanaweza kufaidi kutokana na mapumziko Krismasi.
Si wachezaji na mameneja pekee wanaotatizwa na mechi za kipindi hicho - kuna mashabiki pia
Mashabiki wa Newcastle watasafiri mbali zaidi kwa mechi za Krismasi - takriban maili 964.
Tottenham mashabiki wao nao watasafiri maili 896 - mara tatu zaidi ya umbali wa mashabiki wa Manchester United (maili 288 ) na mara tano zaidi ya mashabiki wa Burnley (maili 160).
Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Watu wenye Ulemavu, Anthony Mavunde, (wa pili kulia) akikabidhi Kombe la SportPesa Super Cup kwa Nahodha wa Gor Mahia, Shakava Haron, baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya AFC Leopards katika mchezo wa fainali uliochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. Na Ripota wa Mafoto Blog, Dar Timu ya Gor Mahia ya Kenya imetwaa ubingwa wa kwanza wa mashindano ya SportPesa Super Cup baada ya kuwasambaratisha wapinzani wao, AFC Leopards kwa mabao 3-0 kwenye uwanja wa Uhuru. Uliozikutanisha timu zote za Kenya uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Kwa ushindi huo, Gor Mahia imepata nafasi ya kupambana na timu maarufu ya Ligi Kuu ya Uingereza, Everton FC Julai 13 kwenye uwanja wa Taifa jijini. Mshambuliaji wa Gor Mahia na mfungaji wa bao la kwanza kati ya matatu, Muguna Kenneth, akimtoka beki wa AFC Leopards, Abdallah Salim, wakati wa mchezo wa Fainali...
Haki miliki ya picha Image caption Korea Kaskazini tayari imelaani mazoezi hayo ikisema kuwa hatua hiyo ni sawa na kumwaga mafuta kwenye moto. Marekani na Korea Kusini wanafanya mazoezi ya kila mwaka ya jeshi, ambayo mara nyingi huighadhabisha Korea Kaskazini licha ya wito wa kutaka mazoezi hayo yasifanyike. Wiki iliyopita Korea Kaskazini ilionekana kulegeza kamba baada ya kutisha kuwa itarusha makombora kwenda kisiwa cha Marekani cha Guam, lakini tena ikasema kuwa itafuatilia mienendo ya Marekani. Korea Kaskazini tayari imelaani mazoezi hayo ikisema kuwa hatua hiyo ni sawa na kumwaga mafuta kwenye moto. Haki miliki ya picha Image caption Mazoezi hayo hujumuisha ya ardhini , baharini na angani China na Urusi mwezi Julai zilipendekeza kusitishwa mazoezi ya kijeshi ili nayo Korea Kaskazini iache kuyafanyia majaribio makombora. Marekani inasema kuwa mazoezi hayo yatawahusisha wanajeshi 17,500 wa Marekani na yatadumu kwa kipindi cha siku kumi. 'Kifaa' cha Korea K...
MSANII wa filamu nchini, Haji Salum maarufu kama Mboto , amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni zinazodai kuwa nguli wa vichekesho katika tasnia ya uigizaji , Amri Athuman maarufu kama King Majuto amefariki dunia. Mboto baada ya kupata taarifa hizi alifunga safari kuelekea mkoani Tanga ambapo ni nyumbani kwa Mzee Majuto na kumkuta hai, na amekanusha uvumi huo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuposti picha inayowaonyesha yeye na Majuto wakiwa nyumbani kwake, na picha hiyo iliambatana na maneno yafuatayo: “ Baada ya kupata taarifa mbaya kuhusu Mzee Majuto nimelazimika kuja kwake Tanga . Ni kweli anaumwa ila anaendelea vizuri na si kama watu walivyozusha kuwa mzee hatunaye. Kwa sasa mzee ni mzima nipo naye Tanga ,” ameandika Mboto . Siku chache zilizopita, gazeti la Ijumaa Wikienda liliripoti taarifa za kuumwa kwa Mzee Majuto...
Comments
Post a Comment