Posts

LORI LAPINDUKA DARAJA MTO SONGWE NA KUZIBA BARABARA

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipenya ili kuvuka katika daraja la mto Songwe kwenye mpaka wa mikoa ya Mbeya na Songwa baada ya Lori lililokuwa limebeba vinywaji baridi kupinduka katika daraja hilo na kuziba barabara. Ajali hiyo ilisababisha msururu mrefu wa magari yaliyokuwa yakitoka Tunduma na yale yaliyokuwa yakitoka Mbeya Julai 24, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu). Msururu wa magari uliosababishwa na ajali ya lori lililopinduka kwenye daraja la mto Songwe katika barabara Mbeya- Tunduma Julai 24, 2017. Lori hilo lilikuwa limebeba vinywaji baridi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

UKWELI KUHUSU MZEE MAJUTO, NA TETESI ZA KUFA

Image
MSANII wa filamu nchini,  Haji Salum maarufu kama Mboto , amekanusha taarifa zinazosambaa mitandaoni  zinazodai kuwa nguli wa  vichekesho  katika tasnia ya  uigizaji , Amri Athuman maarufu kama  King Majuto  amefariki dunia. Mboto baada ya kupata taarifa hizi alifunga safari kuelekea  mkoani  Tanga  ambapo ni nyumbani kwa Mzee Majuto  na kumkuta hai, na amekanusha uvumi huo kupitia ukurasa wake wa  Instagram  kwa kuposti picha inayowaonyesha yeye na  Majuto  wakiwa nyumbani kwake, na picha hiyo iliambatana na maneno yafuatayo: “ Baada ya kupata taarifa mbaya kuhusu  Mzee Majuto  nimelazimika kuja kwake  Tanga . Ni kweli anaumwa ila anaendelea vizuri na si kama watu walivyozusha kuwa mzee hatunaye. Kwa sasa mzee ni mzima nipo naye  Tanga ,” ameandika  Mboto . Siku chache zilizopita,  gazeti la Ijumaa  Wikienda liliripoti taarifa za kuumwa kwa  Mzee Majuto...

Shetta: Mimi ni Chawa Kwa Matajiri Siwezi Kufa Njaa.

Image
Msanii Shetta ametaka watu wasimuhisi kuwa anajishughulisha na biashara za madawa na badala yake watambue yeye ni mtu anayetumia fursa kila aonapo na ndio maana ana marafiki wengi matajiri ambao wanamsaidia. Akizungumza kwenye Planet Bongo East Africa radio, Shetta amesema kwamba yeye hajishughulishi na biashara hizo za madawa na wala hana pesa za kutisha kama jinsi watu wanavyomfikiria. "Mimi sina fedha nyingi kama watu wanavyodhani, sema nina fedha za kutosheleza maisha yangu. Ningekuwa nina pesa nisingwekuwa nawaganda matajiri. Mimi ni chawa kwa matajiri nikiwa nashida namcheki boss Mo, au matajiri ambao nimetengeneza ukaribu nao na mwisho wa siku mambo yangu yanaenda," Shetta. Katika hatua nyingine Sheta amesema yeye ni mtu ambaye anapenda vitu vizuri na ndiyo sababu watu wengi wamekuwa wakimfikiria vibaya 'Ningekuwa nauza madawa ningekuwa na mimi kwenye ile orodha iliyowahi kupelekwa pale polisi. Mimi ni mtu ambaye napenda vitu vizuri na nikikitak...

Wahamiaji Haramu: Kuna siku Tanzania itatawaliwa na mgeni

Image
Baptista Marco raia wa Burundi aliyekamatwa nchini hivi karibuni akifanya kazi kama mwanasheria wa TBS kinyume cha sheria.                  Matukio ya wageni kukamatwa wakifanya kazi nchini–tena nyingine nyeti–kinyume cha sheria yanazidi kuongezeka kiasi cha kuanza kujenga shaka juu ya usalama wa taifa na wananchi kwa ujumla. Hapa lazima tujiulize tatizo liko wapi; na nini kifanyike kuondoa hatari hii ambayo inaweza kutugharimu kama taifa. Wahenga walinena: usipoziba ufa, utajenga ukuta; jambo ambalo ni gharama baada ya nyumba kubomoka.              Kuna matukio ambapo wakimbizi wa kiuchumi wa kigeni wamemeajiriwa nchini na kufanya kazi kwa muda mrefu bila kustukiwa. Je vyombo vyetu wa usalama vinafanya kazi gani na kama vinafanya kazi je vinaifanya vizuri? Mtu anaajiriwa kwa ngazi ya juu. Je anapataje kazi kama hakuna rushwa? Je wako wangapi wahalifu wa namna hii? Je wako peke yao au wan...

Mkataba wa Aishi Manura wavuja ukionyesha kujiunga na simba Simba

Image
MKATABA wa kipa wa Azam FC, Aishi Salum Manula kusaini Simba umevuja kwenye mitandao ya kijamii na unaonyesha mlinda mlango huyo amesaini kwa dau la Sh. Milioni 50 kwa miaka miwili na atakuwa analipwa Milioni 3 kwa mwezi mshahara. Hata hivyo, mkataba huo unasema, Aishi atalipwa kwa awamu fedha hizo, Sh. Milioni 25 wakati wa kusiani, Milioni 5 kabla ya Agosti 30 na Sh. Milioni 20 atamaliziwa kabla ya Desemba mwaka huu. Aishi anakuwa mchezaji wa pili tegemeo wa Azam FC kuhamia Simba SC, baada ya aliyekuwa Nahodha wa timu hiyo ya Chamazi, John Raphael Bocco kutangulia pia Msimbazi kwa dau la Sh. Milioni 50 miaka miwili na mshahara wa Sh. Milioni 4 kwa mwezi. Wachezaji wote wanaondoka Azam FC wakati mikataba yao inamalizika mwishoni mwa mwezi huu na mazungumzo ya kusaini mikataba mipya yalishindikana, kutokana na sera mpya za timu ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake kutotumia fedha nyingi katika kusajili. Aishi aliyesimama langoni jana katik...

GOR MAHIA MABINGWA WA SPORTPESA SUPER CUP 2017, SASA KUKIPIGA NA EVERTON JULAI 13

Image
 Naibu Waziri wa Kazi,Ajira na Watu wenye Ulemavu, Anthony Mavunde, (wa pili kulia) akikabidhi Kombe la SportPesa Super Cup kwa Nahodha wa Gor Mahia, Shakava Haron, baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya AFC Leopards katika mchezo wa fainali uliochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.  Na Ripota wa Mafoto Blog, Dar Timu ya Gor Mahia ya Kenya imetwaa ubingwa wa kwanza wa mashindano ya SportPesa Super Cup baada ya kuwasambaratisha wapinzani wao, AFC Leopards kwa mabao 3-0 kwenye uwanja wa Uhuru.  Uliozikutanisha timu zote za Kenya uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.  Kwa ushindi huo, Gor Mahia imepata nafasi ya kupambana na timu maarufu ya Ligi Kuu ya Uingereza, Everton FC  Julai 13 kwenye uwanja wa Taifa jijini. Mshambuliaji wa Gor Mahia na mfungaji wa bao la kwanza kati ya matatu, Muguna Kenneth, akimtoka beki wa AFC Leopards, Abdallah Salim, wakati wa mchezo wa Fainali...