Raia wa Burundi ''waliotaka kujiunga na al-Shabab'' wamakatwa

Wapiganaji wa al-Shabab nchini Somalia

Image captionWapiganaji wa al-Shabab nchini Somalia
Police nchini Kenya wamewakamata watu wanne wanaoaminika kuwa raia wa Burundi ambao walikuwa wakielekea Somalia kujiunga na kundi la al-Shabab.
Maafisa wa ujasusi walikuwa wakiwafuata washukiwa hao baada ya kupata habari kuhusu mipango yao, kulingana na msemaji wa polisi George Kinoti.
Ameongezea kwamba washukiwa wanne walikamatwa katika kizuizi cha polisi mjini Isiolo takriban kilomita 350 kaskazini mwa mji mkuu wa nairobi wakielekea katika mji wa mpakani wa Mandera.
Maafisa wa polisi pia wanasema wanne hao waliingia nchini Kenya kama watalii kupitia visa huru ya ushirikiano kati ya Burundi na Kenya.
Maafisa katika Ubalozi wa Burundi mjini Nairoibi wanasema kuwa watatoa taarifa kamili kuhusu kukamatwa huko baada ya kushauriana na mamlaka ya Kenya.
Mnamo mwezi Januari mwaka huu raia mwengine wa kigeni, ambaye alikuwa Mtanzania alikamatwa mjini Mandera akijaribu kuvuka na kuingia Somalia kwa lengo la kujiunga na kundi hilo la al-Shabab.

Comments

Popular posts from this blog

GOR MAHIA MABINGWA WA SPORTPESA SUPER CUP 2017, SASA KUKIPIGA NA EVERTON JULAI 13

Marekani na Korea Kusini wafanya mazoezi ya pamoja ya jeshi

UKWELI KUHUSU MZEE MAJUTO, NA TETESI ZA KUFA