Eden Hazard ainusuru Chelsea katika sare ya 3-3 dhidi ya Roma

Eden Hazard akifunga mojawapo ya mabao yake mawaili dhidi ya AS Roma


Image captionEden Hazard akifunga mojawapo ya mabao yake mawaili dhidi ya AS Roma

Eden Hazard aliwaokoa Chelsea's kuendeleza msururu wao wa kutofungwa katika kombe la vilabu bingwa baada ya Roma waliotawala mechi hiyo kutoka nyuma na kuongoza katika kiputi kilichojaa mbwembwe za kila aina katika uwanja wa Stamford Bridge.
Hazard alifunga bao kila kipindi cha mchezo ,mwanzo akifunga kichwa kilichosawazisha matokeo kufuatia krosi ya Pedro zikiwa zimesalia dakika 15 mechi kukamilika katika kundi C.
Mshambuliaji huyo wa Ubelgiji alikuwa ameipatia Chelsea uongozi wa mabao mawili katika kipindi cha kwanza baada ya David Luiz kuiweka Chelsea kifua mbele.
Lakini timu hiyo ya ligi ya Serie A iling'ang'ana huku Aleksandar Kolarov akifunga kabla ya Edin Dzeko kufunga mabao mawili katika dakika sita.
Shambulizi lake la kwanza ulikuwa mpira uliompita kwa juu kipa huku la pili likiwa mchezo mzuri wa nipa ni kupe kati ya Kolarov.

Comments

Popular posts from this blog

Jifunze Jinsi ya kutengeneza sabuni ya Unga na ya maji

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Alexander Lacazette Shujaa wa Arsenal