Rooney ahukumiwa kutoendesha gari kwa miaka miwili



Rooney akiwasili katika mahakama ya Stockport


Image captionRooney akiwasili katika mahakama ya Stockport

Nahodha wa zamani watimu ya taifa ya England Wayne Rooney amehukumiwa kutoendesha gari kwa miaka miwili sambamba na kufanya kazi za jamii kwa saa 100.
Rooney 31, alikamatwa kwenye kitongoji cha Wilmslow, Cheshire kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa Septemba 1.

Rooney anasema kesi hii imeharibu heshima yake kwenye soka
Image captionRooney anasema kesi hii imeharibu heshima yake kwenye soka

Rooney pia atalipa faini ya Pauni 170 kwa kosa hilo.
''Nimekubali kosa langu na nimeomba radhi kwa familia, klabu yangu ya Everton, mwalimu na sasa ni zamu ya mashabiki.Ninaomba radhi kwa kitendo kile.'' alisema Rooney baba wa watoto watatu.

Jaji amemwambia Rooney alijiweka yeye na watumiaji wengine wa barabara katika hatari kubwa
Image captionJaji amemwambia Rooney alijiweka yeye na watumiaji wengine wa barabara katika hatari kubwa

Mchezaji huyo aliyezaliwa katika jiji la Liverpool alijiunga na Everton klabu yake ya utotoni akitokea Manchester United miaka 13 baada ya kuondoka.

Comments

Popular posts from this blog

GOR MAHIA MABINGWA WA SPORTPESA SUPER CUP 2017, SASA KUKIPIGA NA EVERTON JULAI 13

Marekani na Korea Kusini wafanya mazoezi ya pamoja ya jeshi

UKWELI KUHUSU MZEE MAJUTO, NA TETESI ZA KUFA