Posts

Image
Said Alf awakimbia CHADEMA, Ataka ubunge kwa CCM   sos.Mpekuzi blog MBUNGE wa Jimbo la Mpanda Mjini, Bw. Said Amour Alfi (CHADEMA) ni miongoni  mwa makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambao wamechukua na kurejesha fomu za kuomba kugombea ubunge katika Jimbo jipya la Nsimbo, Wilaya ya Mlele, mkoani Katavi kwa tiketi ya CCM kwenye Uchaguzi Mkuu ujao. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu wa CCM mkoani Katavi, Averin Mushi amethibitisha Bw. Arfi kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM katika jimbo hilo.  Alisema makada 23 wamejitokeza kuwania ubunge katika majimbo yote ya uchaguzi mkoani humo ambapo katika Jimbo la Nsimbo, makada ambao wamerejesha fomu ni Bw. Arfi, Shabir Hasanali 'Dallah', Richard Mbogo, Manamba David na Mapesa Frank. Katika Jimbo la Katavi ni Isaack Kamwelwe, Meneja wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoani humo, Shafi Mpenda, Maganga Kampala na Osca Albano. Kwa upande wa Jimbo jipya la Kavuu, yupo Zumb...

Wabunge wa Chadema Wamkaribisha Edward Lowassa

Image
Wabunge wa Chadema Wamkaribisha Edward Lowassa Baadhi ya wabunge wa Chadema wamezungumzia taarifa zinazosambaa zikieleza kuwapo mkakati wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuhamia katika chama hicho, wengi wao wakimkaribisha. Wakati wabunge hao wakikubali kumpokea, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa amesema wananchi wasubiri mambo yatakapokuwa tayari badala ya kutegemea mitandao ya kijamii. “Nitazungumza pale mambo yatakapokuwa sawa, siwezi kuzungumza sasa, subirini… sasa hivi mambo mengi yanazungumzwa kwenye mitandao,” alisema Dk Slaa ambaye pia anatajwa kuwa mgombea wa chama hicho ndani ya Ukawa. Msemaji wa Lowassa, Aboubakary Liongo alipoulizwa kuhusu kuwapo kwa mpango huo alisema hawezi kulizungumzia hilo kwa kuwa ni suala la mtu binafsi. Hata hivyo, jitihada za kumpata Lowassa jana hazikufanikiwa kwani simu yake iliita pasi na kupokewa. Hivi karibuni, idadi kubwa ya madiwani wa CCM walirudisha kadi zao na kujiunga na Chadema wakisem...
Image
CHADEMA Kumtangaza Mgombea Wake wa Urais LEO Jijini Mwanza Dr.Slaa Baada ya vuta vikuvute ya muda mrefu, hatimaye leo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinatarajia kumtangaza mgombea wake wa urais katika mkutano maalumu utakaofanyika jijini Mwanza. Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na viongozi wa chama hicho Kanda ya Ziwa Magharibi na makao makuu zilisema kuwa leo mgombea huyo atatangazwa mkoani hapa huku zikibainisha kuwa anayepewa nafasi kubwa ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa. Taarifa hizo zimekuja wakati kukiwa na tetesi kuwa chama hicho kilikuwa kinafanya mazungumzo na waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliyekuwa anawania urais kupitia CCM na kutemwa katika hatua za awali, huku vyanzo mbalimbali vikisema mazungumzo hayo yanachukua muda mrefu na kuna uwezekano mkubwa wa kutozaa matunda. Jana, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe pamoja na baadhi ya wabunge walikaririwa wakitoa matamko ya kumkaribisha ...

Nchimbi Afunguka baada ya CCM Kulikata Jina lake Kwenye Kinyang'anyiro cha Ubunge

Image
Nchimbi Afunguka baada ya CCM Kulikata Jina lake Kwenye Kinyang'anyiro cha Ubunge Aliyekuwa wazili wa mambo ya ndani na mbunge wa songea mjini Emmanuel Nchimbi akitoa hoja bungeni. Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Songea Mjini, Dk. Emmanuel Nchimbi (pichani), amefunguka kuhusu mambo kadhaa na kueleza kuwa  Watanzania wanapaswa kuelewa kuwa kutofautiana katika vyama vya siasa ni jambo la kawaida katika nchi yenye demokrasia. Dk. Nchimbi alisema hayo jana ikiwa ni siku moja baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Songea Mjini kuikataa fomu ya kuomba kuwania ubunge aliyochukuliwa na wananchi kwa madai haikuwa imekidhi vigezo. “Ninachowambia Watanzania tuzoee kutofautiana, kutofautiana katika vyama vyetu ni jambo la kawaida katika demokrasia, tunaweza kutofautiana katika mapendekezo, lakini tukifika kwenye maamuzi tunakuwa kitu kimoja kuunga maamuzi tuliyoafikiana na huo ndio utaratibu mzuri wa kujenga demokrasi...

Majambazi 27 wenye silaha wakamatwa mkoani Pwani

Image
Majambazi 27 wenye silaha wakamatwa mkoani Pwani Jeshi la polisi Mkoa wa Pwani  limefanya msako mkali katika mapori mbali mbali  na  kufanikiwa kuwakamata   watuhumiwa  wa ujambazi  27 pamoja na   risasi 153,bunduki 2  mabomu 3  ambavyo  walikuwa wakivitumia katika matukio ya uharifu.   Kwa mujibu wa  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina mwandamizi Jafari Ibrahimu amesema kwamba watuhumiwa hao wamekamatwa baada ya kufanyika operesheni katika magenge yaliyopo vichakani na kuwakuta watuhumiwa hao wakiwa wamejificha pamoja na silaha walizokuwa wanazitumia kufanyia uhalifu   Ameongeza kuwa  wameamua kufanya  operesheni  hiyo  kutokana na kuongezeka kwa uharifu katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Pwani na kuwakamata watuhumiwa hao  ambao wengine walikutwa na vifaa mbali mbali ikiwemo visu mapanga,pamoja na nyaya tatu za milipuko ya mabomu.   Kat...

VIDONDA VYA TUMBO.

Image
  VIDONDA VYA TUMBO,DALILI NA MATIBABU YAKE Imekuwa ni changamoto sana kwa watu wanaosumbuliwa na vidonda vya tumbo hii ni kwa sabubu zifuatazo 1.        Jamii haijatambua kuwa vidonda vya tumbo husababishwa na mienendo ya maisha yetu. Hivyo tiba yake kuu ni kubadili maisha tunayoishi nayo,kuanza lishe tunayopata,jamii tunayo ishi nayo, na kuepuka vinywaji vinavyo hatarisha afya ya ukuta wa mfuko wa chakula. 2.        Dawa kama omeprazole na zingine nyingi ambazo kwa pamoja tunaziita PROTON PUMP INHIBITORS zinapunguza utoaji wa asiodi ambayo ikitolewa kwa wingi inaenda kuharibu kuta za mfuko wa chakula. Hivyo zinazuia tu tindikali bila kushugulika na chanzo cha kuongezeka kwa hiyo tindikali. Hivyo bila kuondoa chanzo kinachosababisha kuongezeka kwa tindikali hiyo ya HCL hata siku moja huwezi kupona ndio mana siku hizi kuna dawa za kutuliza kama mmoja wapo wa wagonjwa nilikutana nae anasema hivyo. Inaweza kuwa leo...
Image
WASANII BARNABA NA V.MONEY VANESA Hatimae Aliyekuwa Akitegemewa Kupata Tuzo ya Mtunzi Bora wa Mwaka Kill Awards Mwanamuziki Barnaba Ametoa ya Moyoni Baada ya Kuikosa Tuzo Hiyo: Barnaba - Nawashukuru watu wangu wote na mashabiki Zangu mlionipiga Kura naamini kila kilichotokea Kimestahiri Kutokana Mimi nampenda mungu na naamini kuna Kitu kinaitwa Wakati au muda na napenda Changamoto mana hii Itafanya Nifanye Vyema mara mbili ya pale ninapofanyaga Yes Of coz mimi sinaga Team Bali Team yangu ni wale wote wanaopenda Muziki Mzuri nawapenda wote na nawapa Ongera wenzangu wote mlioshinda Bila kusahau kipenzi Changu #bestfemaleperformer and #bestfemaleartist @Vanessamdee Kushinda kwako ni wazi inaonesha wazi kazi nzuri Aya Tunaendelea na kazi Ya kuangusha Vyuma Juu Ya Vyuma na mwaka Huu natoa #Album Ambayo itafanya Yule asiyemwelewa Barnaba ajue na aelewe mwisho nawakumbusha Umoja ni nguvu utengano............. Tusijenge Matabaka Nndugu zangu