Posts

Vita ya Diamond Platnumz na Alikiba Kuamuliwa Nigeria

Image
Jana usiku majina ya wasanii waliochaguliwa kwenye vipengele mbalimbali vya tuzo za AFRIMA 2017 yametangazwa ambapo kwenye kipengele cha Msanii bora wa kiume kutoka Afrika Mashariki mahasimu Diamond Platnumz na Alikiba wamekutana tena kwenye kipengele hicho na ndiyo Wasanii pekee waliofanikiwa kuingia kwenye kipengele hicho. Wasanii wengine kutoka Tanzania waliotajwa kwenye tuzo hizo ni Lady Jaydee, Nandy na Vanessa Mdee wote wapo kwenye kipengele cha msanii bora wa kike kutoka Afrika Mashariki. Upigaji kura wa Tuzo hizo utaanza Tarehe 21 Agosti mwaka huu na zitatolewa tarehe 12 mwezi Novemba huko Lagos nchini Nigeria, Tazama Orodha kamili ya tuzo za AFRIMA 2017 hapa chini.

Waziri Mwijage Acharuka.......Avifunga Viwanda 10 kwa Kushndwa Kuendelezwa

Image
Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage, amesema serikali imeanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya kutwaa viwanda walivyopewa wawekezaji na kushindwa kuviendeleza huku viwanda vingine vikiwa chini ya uangalizi wa muda Waziri Mwijage amesema hayo jana Mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kikao kilichojumuisha wawakilishi wa Wizara za Fedha, Tamisemi na Wizara ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu. Amevitaja viwanda hivyo kuwa ni kiwanda cha korosho Lindi, Mgodi wa Pugu Kaolin, Mkata Saw Mills Ltd, Manawa Ginnery Co Ltd, Kiwanda cha Chai Dabaga, Tembo Chipboard Ltd, Kiwanda cha Nguo cha Kilimanjaro, Mang’ula Mechanical and Machine Tools co. Ltd na Polysacks cha Dar es Salaam. Aidha, Mhe. Mwijage amesema serikali ambayo awali ilibinafsisha mashirika 341 ya umma ambayo yalijumuisha viwanda, mashamba, makampuni ya biashara, mahoteli na makampuni ya usafirishaji lakini kati ...

Tume ya uchaguzi Kenya yashangazwa na matokeo ya upinzani

Tume ya Uchaguzi ya Kenya imesema ni mapema na ni kinyume cha sheria kwa mgombea wa upinzani Raila Odinga kujitangazia kuwa ameshinda uchaguzi wa Kenya. Alhamisi, muungano wa upinzani wa NASA ulichapisha matokeo ambayo yanaonyesha kuwa Raila Odinga amemshinda Rais wa sasa Uhuru Kenyatta, ambapo pia waliitaka tume ya uchaguzi imtangaze Odinga kuwa ndiye Rais mteule. Hata hivyo matokeo ya awali hadi sasa yaliyotangazwa na tume hiyo yanaonyesha Rais wa sasa Uhuru Kenyatta bado anaongoza dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga. Mwandishi wetu Anne Soy alifanya mahojiano na Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati. Kwanza alimuuliza, je tume hiyo imepokea barua yoyote kutoka upinzani?

Mfumuko wa bei washuka nchini.

Image
Ofisi ya Taifa ya Takwimu imeeleza kuwa mfumuko wa bei nchini kwa kipindi cha Julai mwaka huu umepungua hadi kufikia asilimia 5.2 kutoka asilimia 5.4 iliyokuwapo mwezi Juni mwaka huu hali inayomaanishakasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa imepungua. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii, Ephraim Kwesigabo, amesema kupungua kwa mfumuko wa bei wa kipindi cha Julai mwaka huu kumechangiwa hasa na kupungua kwa baadhi ya bidhaa za vyakula kwa kipindi kilichoishia Julai 2017 ikilinganishwa na bei za Juni 2016. “Baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei ni pamoja na nyama, kwa asilimia 16.6, bilinganya (10.6), vitunguu (13.2), karoti (16.9) na viazi mviringo (13.5)"  amesema. Aidha ameeleza kuwa Shilingi ya Tanzania imezidi kuimarika ambapo uwezo wa Shilingi 100 katika kununua bidhaa na huduma ulifikia Shilingi 91 na senti 87 kipindi cha Julai 2017 ikilinganishwa na shilingi 91 na senti 66 ilivyo...

Korea Kaskazini: Tuna mpango wa kushambulia kisiwa cha Marekani cha Guam siku chache zinazokuja

Image
Haki miliki ya picha Image caption Korea Kaskazini inasema mpango wake ya kufyatua makombora kwenda kisiwa cha Marekani cha Guam Korea Kaskazini inasema mpango wake ya kufyatua makombora kwenda kisiwa cha Marekani cha Guam, utakuwa tayari hivi karibuni huku majibizano ya kivita kati yake na Marekani yakiendelea. Vyombo vya habari vilisema kuwa makombora ya Hwasong-12 yatapita anga ya Japan na kuanguka baharini karibu kilomita 30 kutoka kisiwa cha Guam ikiwa mpango huo utaidhinishwa na Kim Jong-un. Korea ilipuuzna onyo la Donald Trump kuwa itashambuliwa vikali. Marekanai imeionya Korea Kaskazini ikisema kuwa vitendo vyake vinamaanisha kuwa huo utakuwa mwisho wa utawala wa nchi hiyo. Image caption Kisiwa hicho kilicho bahari ya Pacific cha Guam ndiko ziliko kambi za jeshi za Marekani na watu 163,000 Waziri wa ulinzi nchini Marekani Jim Mattis alisema kuwa Korea Kaskazini itashindwa vibaya ikiwa itaingia vitani na Marekani na washirika wake. Korea Kaskazini ilitangaza si...

Uchaguzi Kenya: Matokeo kamili ya urais yasubiriwa

Image
Ni siku ya tatu sasa tangu Wakenya walipofika katika vituo vya kura kuwachagua viongozi na matokeo kamili ya uchaguzi wa urais yanaendelea kusubiriwa Tume ya Uchaguzi inaendelea kupokea Fomu 34A za matokeo ya urais kutoka vituoni Matokeo ya awali yanaonesha Rais Kenyatta anaongoza akiwa na kura 8 milioni. naye Bw Odinga ana kura 6.6 milioni. IEBC imesema mitambo yake haidukuliwa, kinyume na madai ya muungano wa upinzani Nasa Jumanne kulitokea vurugu katika baadhi ya maeneo mtaa wa Mathare, Nairobi na baadhi ya maeneo Kisumu. Lakini kwa sasa hali ni tulivu Waziri wa usalama Fred Matiang'i amewaomba wananchi kuendelea na shughuli za kawaida bila wasiwasi Katika barabara za Nairobi magari yameanza kuonekana lakini bado hali ya kawaida haijarejea Yasemavyo magazeti Kenya leo Imepakiwa mnamo 8:35 Hivi ndivyo magazeti nchini Kenya yalivyoangazia matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Jumanne, hatua ya upinzani kupinga matokeo ya awali yanayotangazwa, kutokea kwa...

Matokeo ya uchaguzi wa urais Kenya

Muungano wa upinzani Nasa umepinga matokeo yanayotangaza na kusema IEBC imekuwa ikitangaza matokeo bila kutoa fomu 34A Kumekuwa wagombea urais wanane, lakini ushindani mkubwa ulikuwa kati ya Rais Kenyatta na Bw Raila Odinga Matokeo yaliyotolewa kufikia sasa yanaonyesha Bw Kenyatta ana kura 7m naye Bw Odinga kura 5.6m. Bw Odinga anawania urais kwa mara ya nne. Kulikuwa na jumla ya vituo 40,883 vya kupigia kura kote nchini Katika matokeo ya vituo 36659 kati ya 40883: Uhuru Kenyatta wa Jubilee ana kura 7,461,933 (54.64%) Raila Odinga wa ODM ana kura 6,079,136 (44.51%) Kura zilizoharibika kufikia sasa ni 353,389.