Posts

Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria aendelea kupata nafuu

Image
Image caption Rais wa Nigeria Bw Muhammadu Buhari Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria ambaye anatibiwa jijini London kwa ugonjwa ambao bado haujatajwa, amezima kimya kirefu na kuzungumza. Kwa njia ya taarifa, Bwana Buhari amesema kuwa "matibabu yanendelea vyema, huku afya yake ikiimarika pakubwa". Hata hivyo, Rais ameongeza kusema kuwa, hata ingawa anajihisi kurejea nyumbani, madakatari bado wakimhudumia, huku akisema sasa ameanza kuzoea kufuata amri na maagizo badala ya kutoa amri. Kimya chake cha muda mrefu, kimezua malumbano kuwa, anafaa arejee Nigeria ama ajiuzulu kiti cha Urais. Tetesi kuhusiana na afya ya Bwana Buhari, imedumu kwa muda mrefu, tangu alipokwenda jijini London kwa matibabu, mwezi Juni mwaka jana. Makamu wa Rais Yemi Osinbajo, amekuwa akitawala Nigeria muda huu wote Buhari akiendelea na matibu.

Uchaguzi Kenya: Tume ya haki za kibinadamu yasema watu 24 wameuawa

Image
Haki miliki ya picha Image caption Wafuasi wa upinzani wamekuwa wakikabiliana na polisi mtaa wa Mathare na Kibera jijini Nairobi na eneo la Kisumu Muungano mkuu wa upinzani nchini Kenya, ambao ulishindwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, umeapa kuendelea na maandamano wenye nia ya kubatilisha kile ambacho unasema kuwa, matokeo "feki" ya uchaguzi mkuu. Mpinzani mkuu wa Bw Kenyatta, Bw Raila Odinga, amedai kuwa uchaguzi huo ulikubwa na wizi mkubwa wa kura. Seneta James Orengo ameiambia BBC kuwa chama chake, kinachoongozwa na Bw Raila Odinga, hakitapinga matokeo ya uchaguzi mkuu mahakamani, huku akisema kuwa Uhuru Kenyatta tayari ametoa vitisho kwa majaji. Kufikia sasa watu 11 wameuawa katika ghasia za baada ya uchaguzi mkuu, ambazo zilianza mara tu baada ya Uhuru Kenyatta kushinda kutangazwa mshindi kwa muhula wa pili mnamo usiku wa kuamkia Jumamosi. Tume ya taifa ya kutetea haki za kibinadamu nchini Kenya, imetoa orodha ya juu ya wahasiriwa wa ghasia hizo huk...

Japan Yapeleka mtambo wa kutibua makombora ya Korea Kaskazini Yatakayorushwa katika Kisiwa cha Marekani.

Image
Japan imepeleka mtambo wa kutibua makombora magharibi mwa taifa hilo kufuatia tishio la Korea Kaskazini kwamba itarusha kombora la masafa marefu katika kisiwa cha Guam nchini Marekani. Mtambo huo kwa Jina PAC3 (Patriot Advanced Capability-3) umepelekwa katika eneo la shimane, Hiroshima na Kochi ambapo Pyongyang( Korea Kaskazini )  inasema kombora lake litapaa kabla ya kuanguka katika maji ya Guam. Jeshi la kulinda baharini la Japan limeripotiwa kutuma mtambo wa kutibua makombora katika bahari ya Japan likiwa na mfumo wa kufuatilia makombora ya masafa marefu.

Kutoka Dodoma Rais Mpya wa TFF ametangazwa rasmi

Image
Kutoka mjini  Dodoma  katika ukumbi wa  St Gasper  ulipofanyika mkutano mkuu wa shirikisho la soka  Tanzania TFF , mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi  Revocatus Kuuli  ametangazwa matokeo ya uchaguzi Mkuu wa  TFF  kwa wajumbe, makamu na Rais wa  TFF . Aliyekuwa makamu wa Rais na kaimu wa Rais wa  TFF   Wallace Karia  ametangazwa rasmi kuwa Rais mpya wa  TFF kwa kupata jumla ya kura 95 na kuwashida  Ally Mayay ,  Emmanuel Kimbe ,  Shija Richard ,  Iman Madega   na  Fredrick Mwakalebela . Kutoka kulia ni Wallace Karia akiteta jambo baada ya kutangazwa  mshindi wa Urais wa TFF Kwa ushindi huo sasa rasmi  Wallace Karia  atatawala nafasi ya Rais wa  TFF  hadi 2021 makamu wake akiwa ni  Michael Richard Wambura   aliyewashinda wagombea wenzake wengine watano. Kama ulipitwa na sera za Wallace Karia wakati wa kampeni zake

Matokeo ya urais ya wagombea wote wanane

Image
mepakiwa mnamo 8:40 Kulikuwa na wagombea wanane katika kinyang'anyiro cha urais nchini Kenya. Matokeo kamili yalikuwa kama ifuatavyo: Ekuru Aukot 27,311 (0.18) Abduba Dida 38,093 (0.25) Cyrus Jirongo 11,705 (0.08) Japheth Kaluyu 16,482 (0.11) Uhuru Kenyatta 8,203,290 (54.27) Michael Wainaina 13,257 (0.09) Joseph Nyagah 42,259 (0.28) Raila Odinga 6,762,224 (44.74) Rais Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee alitangazwa mshindi baada ya kupata kura 8,203,290 sawa na asilimia 54.2 na pia akapata angalau asilimia 25 ya kura katika kaunti 35. Mshindi wa urais huhitajika kupata asilimia 50 ya kura na kura moja zaidi, pamoja na angalau asilimia 25 katika kaunti 24. Baada ya kutangazwa mshindi, alitoa wito kwa mpinzani wake Raila Odinga, ambaye muungano wake uliyakataa matokeo, aungane naye kufanya kazi kwa maslahi ya taifa. ""Sana kwa Raila Odinga, namuomba yeye, wafuasi wake, wote waliochaguliwa kupitia upinzani, tutafanya kazi pamo...

Uchaguzi Kenya 2017: Hali baada ya Kenyatta kutangazwa mshind

Image
   Rais Kenyatta alitangazwa mshindi wa urais Ijumaa usiku baada ya kupata kura 8, 203, 290 sawa na       asilimia 54.2 zilizopigwa Mgombea wa upinzani Raila Odinga alipata kura 6,762,224 sawa na asilimia 44.7 Baada ya matangazo, visa vya maandamano viliripotiwa katika baadhi ya maeneo ambayo ni ngome ya upinzani, mfano Kisumu, Homa Bay na Migori magharibi mwa nchi hiyo Kulitokea pia visa vya maandamano na polisi kufyatua gesi ya kutoza machozi katika baadhi ya mitaa jijini Nairobi      Hali ya kawaida yarejea Garissa Imepakiwa mnamo 9:33 Hali ya kawaida imeanza kurejea mjini Garissa siku moja baada ya matokeo ya uchaguzi wa urais kutangazwa. Sehemu ya soko kuu mjini humo iliteketezwa Jumatano wakati wa ghasia kati ya wafuasi wa wagombea wawili wa ugavana. Lakini jana na leo hali imekuwa tulivu. Mwandishi wetu Bashkas Jugsodaay amepiga picha hizi za wananchi wakiendelea na shughuli zao za kawaida leo asubuhi.

Vita ya Diamond Platnumz na Alikiba Kuamuliwa Nigeria

Image
Jana usiku majina ya wasanii waliochaguliwa kwenye vipengele mbalimbali vya tuzo za AFRIMA 2017 yametangazwa ambapo kwenye kipengele cha Msanii bora wa kiume kutoka Afrika Mashariki mahasimu Diamond Platnumz na Alikiba wamekutana tena kwenye kipengele hicho na ndiyo Wasanii pekee waliofanikiwa kuingia kwenye kipengele hicho. Wasanii wengine kutoka Tanzania waliotajwa kwenye tuzo hizo ni Lady Jaydee, Nandy na Vanessa Mdee wote wapo kwenye kipengele cha msanii bora wa kike kutoka Afrika Mashariki. Upigaji kura wa Tuzo hizo utaanza Tarehe 21 Agosti mwaka huu na zitatolewa tarehe 12 mwezi Novemba huko Lagos nchini Nigeria, Tazama Orodha kamili ya tuzo za AFRIMA 2017 hapa chini.