Posts

SIMBA VS YANGA NANI KULIA NANI KUCHEKA?, HII NI MECHI YA 'UTATOA HUTOI' TUKUTANE KESHO TAIFA

Image
 *Huku Ajib, Tshishimbi na Ngoma   *Kule Okwi, Niyonzima na Gyan *Matokeo yatadhihirisha usajili wa vikosi bora kati ya Lwandamina na Omog MATOKEO YA MECHI ZA NGAO YA JAMII 2008- Yanga 2-Simba 1 2009- Mtibwa Sugar 1- Yanga 0 2010- Yanga 0- Simba -ikapigwa mikwaju ya penati, Yanga 3-Simba 1 2001- Simba 2- Yanga 0 2012- Simba 3- Azam 2 2013- Yanga 1- Azam 0 2014- Yanga 3- Azam 0 2015- Yanga 2- Azam 2 ikapigwa mikwaju ya penati, Yanga 8- Azam 7 2016- Azam  4- Yanga 1 2017- Yanga ?- Simba ? Na Abdul Dunia, Dar KUMBUKUMBU zinanirudisha miaka mitatu nyuma. Kilinukishwa pale Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Ilikuwa bonge la mechi kali  isiyo na mfanowe. Katika dakika 90 za mtanange huo yalishuhudiwa mabao sita. Hakika ilikuwa mechi ya haja. Yalitokea matukio kibao katika mtanange huo ikiwa ni pamoja na baadhi ya mashabiki kuzimia. Wachezaji walitaharuki, maaskari na  matabibu wa huduma ya kwanza wote walikuwa bize siku h...

Idadi ya watoto wanaotumiwa kama walipuaji wa kujitolea mhanga yaongezeka Nigeria

Image
Haki miliki ya picha Image caption The Boko Haram insurgency has devastated many lives across north-eastern Nigeria Kumekuwa na ongezeko kwa idadi ya watoto wanaotuimiwa kama washambuliaji wa kujitolea mhanga na wanamgambo wa Boko Haram, kaskazini mashariki mwa Nigeria, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto Unicef, linasema kuwa tayari visa 83 vimeripotiwa mwaka huu, mara nne zaidi ya vile vya mwaka wote wa 2016. 55 kati yao walikuwa ni wasichana walio na umri chini ya miaka 15 na kwenye kisa kimoja, bomu lilifungwa kwa mtot ambaye alikuwa amebewa na msichana mdogo. Unicef inasema mbinu hii imezua hofu kwa watoto wanaoachiliwa na Boko Haram. Kulingana na Umoja wa Mataifa, watoto 127 wametumiwa kama walipuaji kaskazini mashariki mwa Nigeria tangu mwaka 2014. Wanamgambo wa Boko Haram mara kwa mara wamewatumia watoto, na wamewateka mamia ya wasichana wa shule na kuwalazimisha watoto wavulana kujiunga na jeshi lao.

Marekani yawekea vikwazo makampuni ya China na Urusi

Image
Haki miliki ya picha Image caption Korea inasisitiza kuwa ina haki ya kuwa na mpango wa nyuklia kwa usalama wake Marekani imetangaza vikwazo kwa kampuni kadha za Urusi na Uchina na watu ambao inawalaumu kwa kusaidia mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini. Hii inajiri baada ya baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa, zikiwemo Urusi na China kupiga kura ya kuiwekea viwazo zaidi Korea Kaskazini. Wizara ya fedha nchini Marekani ilisema kuwa vikwazo hivyo vitaongeza shinikizo kwa Korea Kaskazini lakini hatua hiyo imeighadhabisha China. Haki miliki ya picha Image caption Korea Kaskazini inapinga mazoezi ya pamoja kati ya Korea Kusini na Marekani Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani Rex Tilleron, wakati huo huo ameipongeza Korea Kaskazini kwa kujizuia siku za hivi karibuni. "Hatujashuhudia urushaji wa makombora na vitendo vya uchokozi kutoka Korea Kaskazini tangu azimio la baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa lianze kutekelezwa," alisema. Wizara ya fedha ...

PICHA 13: Rais wa Zanzibar alivyozindua Madarasa katika Skuli ya Msingi Kijitoupele.

Image
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Ali Mohamed Shein August 21, 2017 aliweka Jiwe la Msingi kuzindua madarasa matatu yaliyojengwa kwa Siku 11 chini ya Kampeni ya ‘Mimi na Wewe’ inayosimamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Maghalibi Ayub Mohammed Mahmoud.

Trump aapa kuwa atashinda vita Afghanistan

Image
Image caption Trump amesema ataongeza idadi ya wanajeshi Afghanistan Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa kuondolewa kwa wanajeshi wa Marekani kutoka nchini Afghanistan kutaacha pengo ambalo huenda likajazwa na magaidi. Alisema kuwa mapango yake ilikuwa ni ya kuondoa vikosi vya Marekani, lakini badala yake ameamua wanajeshi hao kubakia ili kuzuia kurudia makosa ambao yalitokea nchini Iraq. Amesema pia kuwa anaongeza idadi ya wanajeshi watakao pelekwa nchini Afghanstan. Akizungumza kupitia Televishen, Rais Trump amesisitiza kuwa kipaumbele cha Marekani ni kutekeleza masuala yenye maslahi katika usalama wa taifa hilo, kutokomeza mtandao wa ugaidi. Image caption Trump amesema ni vigumu kuwaondoa wanajeshi wa Marekani nchini humo Amesisitiza pia kuwa kitendo cha Marekani kujiondoa kwa haraka Afghanistan, kitatatoa mwanya kwa ugaidi kujiimarisha zaidi kama ilivyotokea Iraq. Hata hivyo Trump amekwepa kuzungumzia moja kwa moja muda wa mwisho wa ushiriki wa Marekani nc...