Posts

Rais Magufuli atangaza uamuzi mgumu Mererani

Image
Mererani. Rais John Magufuli ameliagiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kujenga uzio kuzunguka machimbo ya Tanzanite Mererani, hatua ambayo imepokewa kwa hisia tofauti na wananchi wa eneo hilo. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa barabara mpya ya lami kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) hadi Mererani, yenye urefu wa kilomita 26, iliyogharimu Sh32.5 bilioni, Rais Magufuli alisema lengo la mpango huo ni kudhibiti wizi na utoroshwaji wa madini ya Tanzanite. Rais Magufuli aliagiza kuanza haraka kwa ujenzi huo kuzunguka eneo lote la migodi kuanzia Kitalu A hadi D lenye ukubwa wa kilomita za mraba kati ya 13 hadi 14 kwa kuwa ndilo lenye uzalishaji mkubwa wa Tanzanite. “Lile eneo la Kitalu A hadi D ambalo ndilo lina mali nyingi ya Tanzanite naagiza Jeshi la Wananchi kupitia Suma JKT na wengine, najua wamekwishamaliza utafiti, waanze kujenga ukuta wataweka kamera na patakuwa na mlango mmoja, vifaa maalumu vya ukaguzi, wewe ukiweka Tanzanite tumb...

Sugu Amjibu Faiza Ally na Kuweka Mpaka Risiti Alizolipia Ada ya Mtoto..Faiza Amshukia Tena

Image
SUGU: Huwa sipendi kupost mambo haya lakini imenibidi, hizi ni bank slips za ada ya mwisho niliyolipa kwenye shule ya kindergarten aliyokuwa anasoma mwanangu za mwezi wa 5 mwaka huu 2017 ambako alishamaliza . Na mwezi huu wa 9 ilikuwa nimuanzishe shule Feza Nursery pale Mikocheni, lakini from no where mama yake ghafla akanizuia na kusema ahitaji tena nilipe ada na hata kunizuia nisimuone tena Sasha! Na kwamba ana uwezo wa kumpeleka shule anayotaka yeye na ndio akampeleka huko Hazina International, ambako pia hata hivyo nilishaanza kuwasiliana na uongozi ili niendelee tu kulipa ada hata kama nimepigwa marufuku kumuona mwanangu bila sababu... # Hivi kama ni nyie mngefanyaje ? Na nyie mnaotukana ovyo mitandaoni bila kuwa na ukweli mnaoujua tafadhali sana naomba hebu kwanza KABILIANENI NA HALI ZENU kwenye maisha... Asanteni FAIZA ALLY: We baba mjing* lol angalieni risiti za mwaka gani na sasha alianza kusoma lini ? Ka***mbe mbele na sita kuacha mpaka unyooke ! Mnafki mkub...

BREAKING: Mipango ya kumpeleka Tundu Lissu Marekani yasimamishwa

Image
Kulikua na mipango ya kumpeleka Marekani Mwanasheria Mkuu wa  CHADEMA   Tundu Lissu  ambae amekua akitibiwa Nairobi Kenya kutokana na majeraha ya risasi alizopigwa Dodoma September 7 2017. Mipango ya kumpeleka Marekani ilikua ni kwa ajili ya kumpatia matibabu bora zaidi chini ya Hospitali yenye uwezo mkubwa wa Madaktari na teknolojia lakini mipango hiyo imefutwa kwa sasa kutokana na ushauri wa Madaktari wa Hospitali alikolazwa Kenya. Bonyeza play hapa chini kupata undani wa hii taarifa……

Bondia Jake LaMotta afariki akiwa na miaka 95

Image
Image caption LaMotta alikuwa mpiganaji na mchekeshaji Bondia wa zamani wa uzito wa kati na mchekeshaji Jake LaMotta,amefariki dunia akiwa na miaka 95. Mke wake amesema LaMotta amefariki nyumbani kwake kwa ugonjwa wa homa ya mapafu. Alikuwa mpiganaji maarufu zaidi miaka ya 40 na 50. Image caption LaMotta enzi za upiganaji Atakumbukwa kwa uvaaji wa kaptula yenye mistari ya chuichui na wakati fulani alikua akiingiza uchekeshaji wakati akipigana jambo lililomfanya mpinzani wake kuishia kucheka na yeye kushinda.

Juhudi za uokoaji zinaendelea Mexico

Image
Haki miliki ya picha REUTERS Image caption Juhudi za Uokoaji zikiendelea Juhudi za kuwatafuta waliofukiwa na kifusi kufuatia Tetemeko kubwa la ardhi lililoikumba Mexico zinaendelea licha ya matumaini madogo, kuwakuta hai. Wafanyakazi wa majanga ya dharura na wale wa kujitolewa wamekuwa wakichimbua vifusi kwa kutumia mikono. Watu 225 wamefariki nchi nzima kutokana na tetemeko hilo, wakiwemo watoto 21, ambao walikufa wakiwa shuleni Mexico city. Kuna hofu ya watoto zaidi kufariki kutokana na kwamba walikuwa darasani jengo lilipo poromoka. Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto amesema kila dakika inahesabika katika kuokoa maisha ya watu. Watu 52 tayari wameokolewa kutoka katika kufusi katika mji mkuu wa nchi hiyo. Tetemeko hilo la ardhi ni la pili kuikumba nchi hiyo katika kipindi cha mwezi mmoja.

Mtoto aliyehai agunduliwa kifusini

Image
Haki miliki ya picha AUTHORITY Image caption juhudi za uokoaji zikiendelea Waokoaji katika mji wa Mexico city wanajaribu kumfikia msichana mdogo, aliye hai chini ya kifusi cha jengo la shule, lililoporomoka wakati wa Tetemeko la ardhi lililotokea jana. Wamekuwa wakimpitishia chakula na maji, wakati wakijaribu njia ya kuweza kumtoa salama kutoka katika maangamizi hayo. Watoto wapatao 21 wamekufa baada ya jengo walilokuwamo kuvunjika, huku wengine wakiwa bado ndani ya kifusi hicho. Haki miliki ya picha EPA Image caption Wengine tetemeko liliwakuta wakiwa kanisani Jumla ya watu mia mbili na 25 wamefariki kutokana na tetemeko hilo. Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto amesema kila dakika imekuwa ikihesabika katika kuokoa maisha. Tetemeko hilo la ardhi ni la pili kuipiga nchi hiyo mwezi huu.

Kimbunga Maria: Kisiwa chote cha Puerto Rico hakina umeme

Image
Haki miliki ya picha AFP/GETTY IMAGES Image caption Kimbunga Maria kimekata umeme katika kisiwa chote cha Puerto Rico, chenye watu milioni 3.5 Kimbunga Maria kimekata umeme katika kisiwa chote cha Puerto Rico, chenye watu milioni 3.5. Abner Gómez, ambaye ni mkuu wa utoaji huduma za dharura alisema kuwqa hakuna mtu anayetumia umeme aliye na huduma hiyo kwa sasa. Kituo cha vimbunga cha Marekani kinasema kuwa mafuriko makubwa yanaikumba nchi hyo. Maria kwa sasa kinaondoka nchini Puerto Rico na kumepunguza nguvu zake hadi kiwango cha pili. Haki miliki ya picha REUTERS Image caption Kimbunga Maria kimekata umeme katika kisiwa chote cha Puerto Rico, chenye watu milioni 3.5 Baada ya kimbunga Maria kuipiga Puerto Rico, gavana ameamrisha watu kusalia manyumbani mwao kuanzia saa kumi na mbili jioni na hadi saa kumi na mbili asubuhi. Hi ni hatua ya kuwazuia watu kupata ajali kutokana na nyaya za umeme zilizoanguka na vifuzi vilivyo barabara za mji. Mapema Bw Rossello alimuo...