Posts

Nini siri ya mafanikio ya CCM Tanzania?

Image
Haki miliki ya picha AFP/GETTY Shughuli ya kusukwa upya kwa safu ya uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania itahitimishwa wiki hii katika mkutano mkuu unaofanyika mjini Dodoma, katikati mwa nchi hiyo. Huu ni uchaguzi wa kwanza tangu Rais John Magufuli aliporithi uenyekiti kutoka kwa mtangulizi wake, Jakaya Kikwete.  CCM inaendeleza mikakati ya kurejesha hadhi yake baada ya ushindi uchaguzi wa mwaka 2015. Licha ya kushinda urais kwa taabu, wapinzani chini ya mwamvuli wa UKAWA walipata karibu theluthi moja ya viti vyote vya ubunge na kudhibiti halmashauri katika miji muhimu ikiwemo Dar es Salaam, hii ikiwa ni rekodi mpya.  Miaka miwili ndani ya utawala wa Rais Magufuli, upepo unaonekana kugeuka. Upinzani unaelekea kudhoofika, wakati CCM ikiimarika na kung'ara miongoni vyama vya ukombozi vilivyoleta uhuru katika nchi zao.  Ingawa haikuwepo wakati wa uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 wala mapinduzi ya Zanzibar 1964, CCM inahesabika kama chama cha uko...

Polisi India wafunga akaunti ya mtuhumiwa wa mauaji

Image
Image caption Shambhu Lal katika picha inayomuonyesha akimnyanyasa mtu huyo Polisi katika jimbo la Rajasthan nchini India wamefunga akaunti ya benki ya mtu anayehusishwa na mauaji ya muislamu mmoja. Inasema zaidi ya dola elfu nne zilishachangiwa kwenye akaunti yake kabla ya kufungiwa. Shambhu Lal muumini wa dhehebu la Hindu anatuhumiwa kumuua mtu huyo na kutuma picha katika mitandao ya kijamii. Polisi inasema zaidi ya watu mia saba wamechangia akaunti yake. Video hiyo inamuonyesha Shambhu Lal akimlazimisha mtu huyo kuingia dhehebu la Kihindu kabla ya baadae kutuma picha akiwa amefariki.

Dereva aliyesababisha ajali ya gari la shule kuhojiwa Ufaransa

Image
Image caption Ajali hiyo ilitokea karibia na eneo la shule Wapelelezi nchini Ufaransa wanasubiria kumuhoji mwanamke dereva wa gari la shule lililogonga treni karibu na Perpignan Mashariki mwa nchi hiyo na kusababisha vifo vya watoto wanne. Amepata majeraha kadhaa. Waziri mkuu wa Ufaransa Edouard Philippe aliyekwenda eneo la tukio amesema watu 11 wapo katika hali mbaya. Wengine tisa walijeruhiwa kidogo. Amesema kazi ya kuwatambua majeruhi imekua ngumu. Gari hilo lilikuwa ndio limepakiwa wanafunzi hao muda mfupi na lilitembea mwendo wa kilomita moja tu kabla ya ajali hiyo.

Tanzania yajitenga na Trump kuhusu Jerusalem

Image
Haki miliki ya picha AFP Image caption Mji wa Jerusalem una maeneo matakatifu kwa Waislamu, Wakristo na Wayahudi Tanzania imesema haikubaliani na hatua ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kuutambua mji wa Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel. Wizara ya mambo ya nje ya Tanzania kupitia taarifa imesema nchi hiyo inaunga mkono makubaliano ya kimataifa ambayo yanatambua haki ya watu wa Palestina kumiliki Mashariki mwa Jerusalem kama ilivyokuwa kwenye mpaka wa kabla ya mwaka 1967. "Tanzania inaunga mkono msimamo wa Umoja wa Mataifa wa suluhu ya mataifa mawili ambayo unatoa nafasi ya Israel na Palestina kuwepo kwa pamoja zikiwa na mipaka salama," taarifa hiyo iliyotuwa saini na Waziri Augustine Mahiga imesema. Bw Trump kando na kuitambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel, alisema nchi hiyo pia itahamisha ubalozi wake kutoka Tel Aviv. Bw Mahiga amesema ubalozi wa Tanzania utaendelea kuwepo mjini Tel Aviv. Msimamo wa Tanzania unaenda sambamba na msimamo wa mataifa mengi ...

Furry ataka kuzipiga na Anthony Joshua

Image
Image caption Furry ni miongoni mwa mabondia wa Uingereza waliotamba mwaka 2015 Bondia wa uzito wa juu wa Uingereza Tyson Fury ametaka kupewa pambano la haraka baada ya kurejea tena katika ndondi. Fury aliyefungiwa kushiriki mchezo huo mwaka 2016 kwa sababu sampuli zake zilisemekana kuonyesha kutumia dawa za kusisimua misuli, ametaka pia kurudishiwa mikanda yake mara moja. Bondia huyo mwenye miaka 29 tiyari ameonyesha nia ya kupambana na mkali wa uzito wa juu Anthony Joshua mwaka 2018. Promota wa Joshua, Eddie Hearn amesema ni jambo jema na anaamini Furry atachapwa ndani ya raundi tano. Furry alipatikana na hatia ya kutumia dawa zilizokataliwa michezoni na kwa sasa adhabu yake inafikia ukingoni.

Mwanamke aliyejaribu kuwauza watoto wake pacha akamatwa Nigeria

Image
Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Mwaka 2013 wasichana wajawazito 17 na watoto 11 waliokolewa wakati polisi walivamia "kiwanda cha watoto" katika jimbo la Imo Mwanamke mmoja amekamatwa baada ya madai kuwa alijaribu kuwauza watoto wake pacha wenye umri wa mwezi mmoja nchini Nigeria. Ameshtaki kwa kuhusika katika bishara ya kuuza watoto lakini polisi wanasema kuwa mashtaka zaidi yataongezwa. Mwanamke huyo alikamatwa wakati akijaribu kuuza watoto wake wasicha kwa dola 980 kwa mnunuzi ambaye aliwajulisha polisi. Visa vya kuuzwa watoto wa kupangwa vimekuwa tatizo kwa muda mrefu chini Nigeria. Image caption Nigeria ni mzalishaji mkuwa wa mafuta lakini asilimia kubwa ya watu milioni 170 wanaishi kwenye umaskini. Alipohojiwa mwanamke huyo alisema kuwa changamoto za kifedha zilisababisha afanye hivyo. Nigeria ni mzalishaji mkuwa wa mafuta lakini asilimia kubwa ya watu milioni 170 wanaishi kwenye umaskini. Mwaka 2013 wasichana wajawazito 17 na watoto 1...

Mwanamke aliyemuua mume wake ili aishi na mpenzi wake India

Image
Image caption Swati Reddy (kulia) na mpenzi wake wanadaiwa kumuua mume wake Sudhakar (kushoto) mwezi uliopita Wapenzi wiwili nchini India wamekamatwa kwa kumuua mume wa mwanamke na kisha kujaribu kumfanyia upasuaji wa kubadilisha sura mwanamume mpenzi ili aweze kuchukua mahala pake, Tindi kali ilimwagwa kwenye uso wa mwanamume, mpenzi wa mwanamkea, katika shambulizi lililopangwa, huku wapenzi hao wakipanga kusema kuwa sura yake ilikuwa imebadilika baada ya upasuaji. Lakini ndugu wa bwana wa mwanamke aligundua mpango huo alipofika hospitalini. Alitoa malalamiko yake kwa polisi ambao walifanya uchunguzi wa vidole na kugundua njama huyo. Mke, Swati Reddy amekamatwa. Polisi waliiambia BBC kuwa watamkamata pia mpenzi wake, Rajesh Ajjakolu mara atakapotibiwa majeraha yake na kuruhusiwa kuondoka hospitalini. Image caption Rajesh Ajjakolu alilazwa hospitalini akiwa na majeraha ya uso Bwana Sudhakar Reddy anadaiwa kuuliwa usiku wa tarehe 26 Novemba na mwili wake kutupwa siku i...