Los Angeles kuandaa Olimpiki 2028


Carl Lewis
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionCarl Lewis
Jimbo la Los Angeles limeteuliwa rasmi kuandaa mashindano ya Olimpiki ya wakati wa majira ya joto mwaka 2028 katika makubaliano yatakayoihakikishia Paris kuandaa Olympiki ya mwaka 2024.
Miji yote miwili ilikuwa akipigania kuwa mwenyeji wa mashindano hayo makubwa duniani katika tarehe za awali.
Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki Thomas Bach amesema anakaribisha uamuzi huo wa Los Angeles kukubali kuwa mwenyeji wa mashindano hayo kwa tarehe za mbele.
Kamati hiyo ya Olimpiki imesema itatoa mchango wake wenye thamani ya dola bilioni 0.8 kwa mji wa Los Angeles ili kufidia gharama zitakazoongezeka.

Comments

Popular posts from this blog

Jifunze Jinsi ya kutengeneza sabuni ya Unga na ya maji

Jinsi ya kutengeneza SABUNI ya kipande YA KUGANDISHA

Alexander Lacazette Shujaa wa Arsenal