Posts

“Ukibisha kapambane na kulipa mishahara wachezaji wako”-Haji Manara

Image
Mkuu wa  idara  ya habari na mawasiliano wa club ya Simba Haji Manara ni moja kati ya viongozi na wapenzi wa soka wanaojiamini sana na mara nyingi amekuwa akipenda kuandika post za utani kwa wapinzani wao Yanga. Haji Manara usiku huu kutoka katika instagram account yae ameandika ujumbe akiwa kapost picha ya kikosi  cha Simba kuwa kwa sasa Simba ndio Brand maarufu zaidi nchini kuliko zote, unaweza andika comment yako hapo chini.

Ally kiba kawajibu mnaosema kaiba wimbo wa ‘SEDUCE ME’

Image
Usiku wa September 9, 2017 Fiesta ilifanyika kwa mara ya kwanza jijini Arusha ambapo wasanii mbalimbali walitumbuiza kwenye stage na miongoni mwao ni msanii anayefanya muziki wa bongofleva Alikiba ambaye alipata nafasi ya kuzungumza na kituo cha Ayo Tv na kuelezea kuhusu kudaiwa kuiba wimbo wa   ‘Seduce me’ . Alikiba amesema kuwa sikweli kuhusu kudaiwa kuiba wimbo huo bali ni wimbo wake na hana tabia za kuchukua wimbo wa mtu japo amedai wimbo wake kwa sasa unafanya vizuri kwa kuwa ni mzuri. Bonyeza  PLAY  hapa chini kumsikia  Alikiba  akizungumza kila kitu chanzo AYO TV

Wapiganaji wa Rohingya watangaza kusitisha mapigano, Myanmar

Image
Haki miliki ya picha EPA Image caption Wa Rohingya wanaishutumu jeshi la Myanmar kwa kuteketeza vijiji vyao - Lakini utawala nchini Myanmar, unasema wanajeshi wake wanakabiliana na "magaidi" Katika taarifa nyingine Asubuhi hii ya leo, waasi wa kiislamu wa kabila la Rohingya nchini Myanmar wametangaza upande mmoja makubaliano ya kusitisha mapigano leo Jumapili, ili kujaribu kupunguza mgogoro wa kibinadamu magharibi mwa taifa hilo. Mashambulio dhidi ya jeshi la taifa hilo yanayotekelezwa wapiganaji wa Arakan Rohingya Salvation Army, yalisababisha mapigano makali ya wiki mbili, ambapo zaidi ya watu laki tatu wa jamii ndogo ya Warohingya wamekimbilia nchi jirani la Bangladesh.  Image caption Ramani ya Myanmar Kundi hilo la waasi, yameiomba jeshi la nchi hiyo pia kuitisha wito wa kusitisha mapigano, huku likiomba mashirika ya utoaaji misaada ya kibinadamu kurejelea kazi zao za kusambaza misaada. Waziri mmoja wa serikali ya Myanmar ameiambia BBC kuwa, wengi wa Wa-Rohi...

Kimbunga Irma chakaribia Florida

Image
Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Upepo mkali wa kimbunga Irma kimeanza kushuhudiwa Florida Nguvu ya upepo mkali unaondamana na kimbunga, kimeanza kugonga visiwa kadhaa kusini mwa jimbo la Florida nchini Marekani, huku kimbunga kikiacha uharibifu mkubwa katika visiwa vilivyoko kwenye bahari ya Atlantic huko Caribbean, kuelekea Marekani. Kimbunga Irma, kinatarajiwa kugonga maeneo hayo, baadaye leo Jumapili. Viwango vya maji tayari vimeanza kuogezeka katika maeneo ya pwani ya Florida, eneo ambalo linatarajia kimbunga kikubwa kuwasili. Taharuki na hatma ya baadaye ya mji wa Tampa, ambao unakabiliana ana kwa ana na njia inakopitia kimbunga hicho, haijulikani. Image caption Ramani ya mwendo wa Kimbunga Irma Tampa inasemekana kuwa ni mji ulioko katika mazingira magumu zaidi nchini Marekani, hasa kuhusiana na hatari ya kugongwa mara kwa mara na vimbunga. Zaidi ya watu milioni 6 huko Florida wanaondolewa majumbani mwao- robo tatu ya idadi nzima ya watu wa jimbo ...

Madaktari watoa meno 7 kutoka kwa mtoto wa mwezi mmoja India

Image
Image caption Madaktai watoa meno 7 kutoka kwa mtoto wa mwezi mmoja India Madaktari kwenye hospitali moja iliyo jimbo la magharibi mwa Inida ya Gujarat wamefanikiwa kutoa meno saba kutoka kwa mtoto wa mwezi mmoja. "Kwa sasa mtoto yuko sawa," daktari ambaye alifanya upasuaji huo Meet Ramatri alisema. Alisema kuwa upasuiji huo ulifanya kwa njia mbili. Kwanza walitoa meno manne, na baadaye matatu. Meno ya mtoto huyo yaligundulwia siku chache baada ya kuzaliwa. Wazazi wake walimpeleka kwa daktari wakati alipata matatizo ya kunyonya, Image caption Madaktai watoa meno 7 kutoka kwa mtoto wa mwezi mmoja India Baada ya kumfanyia uchunguzi dakari aligundua nyama nyeupe na kumtuma kwa daktari Ramatri. "Wakati nilimfanyia uchunguzi aligundua meno saba," Dr Ramatri aliambia BBC. Kisha alilazimika kutoa meno hayo kwa njia ya upasuajia. "Sasa mtoto huyo anaweza kunyonya," dakatari alisema, lakini aliongeza kuwa ni vigumu kujua ikiwa upasuaji huo ...

Gwiji wa muziki wa country Don Williams afariki dunia

Image
Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Don Williams alianza kuimba muziki kama mwanamuziki wa kujitegemea mwaka 1971 Mwanamuziki nyota wa nyimbo za mtindo wa country kutoka Marekani Don Williams amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 78. Mzaliwa huyo wa jimbo la Texas amefariki baada ya kuugua kwa muda mfupi, afisa anayesimamia mawasiliano yake ametangaza. Williams alianza kuimba nyimbo kama mwanamuziki wa kujitegemea mwaka 1971, na tangu wakati huo alichomoa nyimbo 17 zilizogonga chati za muziki wa country. Nyimbo zake zilizovuma zaidi ni pamoja na  Gypsy Woman  na  Tulsa Time , ambazo ziliimbwa tena na wanamuziki wengine kama vile Eric Clapton na Pete Townshend. Williams alitazamwa na wengi kama gwiji mnyenyekevu wa muziki wa country. Nyimbo zake nyingine zilizovuma ni pamoja na  You're My Best Friend, I Believe in You  na  Lord, I Hope This Day Is Good . Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Troy Gentry alikuwa amepang...

Kimbunga Irma chawasili Cuba

Image
Haki miliki ya picha REUTERS Image caption Kimbunga Irma kikiandamana na upepo mkali. Kimbunga hicho ambacho kimeendelea kuimarika saa chace zilizopita kinatarajiwa kuathiri miji ya pwani. Kifikia sasa watu ishirini wamerikpotiwa kufariki katika visiwa vya Carebean. Msemaji wa kituo cha kushughulikia majanga, nchini Marekani,amesema kimbunga hicho huenda kika-muangamiza mtu yeyeyote ambaye hatajiepusha nacho.  Kumeshuhudiwa msongamano mkubwa wa magari na upungufu wa petroli, wakaazi wa Florida wakielekea maeneo ya kaskazini. Wakati huo huo kimbunga Ema kinachoendelea kusonga kwa kasi,sasa kimeingia nchini Cuba.  Kimbunga hicho, kinaandamana na upepo mkali na mvua kubwa kuelekea visiwa vya kaskazi mwa Caribbean. Bahamas hata hivyo imenusurika na kimbunga hicho baada ya upepo kubadilisha mkondo. Visiwa vya mashariki vilivyokuwa vimekumbwa na mafuriko makubwa sasa ya yanakabiliwa na tishio la kugongwa na kimbunga kingine. Shughuli ya kuwaondoa watu kati...