Burundi hali si Shwari; Amnesty International

Amnesty



Image captionAmnesty International limeonya juu ya usalama wa wakimbizi wa Burundi wanaorudi nchini kwao kutoka Tanzania

Shirika la kimataifa linalotetea haki za binadamu la Amnesty International limeonya kuwa Maelfu ya wakimbizi wa Burundi wanaorudi nchini kwao kutoka Tanzania wanakabiliwa na hatari za kiusalama nchini mwao. 
Mwezi uliopita, Tanzania, Burundi na shirika la umoja wa mataifa linalohudumia wakimbizi UNHCR walikubaliana kwamba kufikia mwisho wa mwaka huu wawe wamewarejesha wakimbizi elfu kumi na mbili wanaoishi Tanzania na wanataka kurudi kwao Burundi kwa hiari. 
Lakini Amnesty International linasema, mpango huu unahatarisha maisha ya maelfu ya wakimbizi na linaamini kuwa wakimbizi wengi wanarejeshwa nyumbani kwao kutokana msukumo wa ushawishi kutoka serikali ya Tanzania na Burundi.
Shirika hilo limedai kuwa hali ya usalama bado sio shwari katika ripoti yao inayotoka leo, wanasema visa vya kuteswa, kufungwa bila makosa, kubakwa na hata kuuwawa bado vinaendelea.

Comments

Popular posts from this blog

GOR MAHIA MABINGWA WA SPORTPESA SUPER CUP 2017, SASA KUKIPIGA NA EVERTON JULAI 13

Marekani na Korea Kusini wafanya mazoezi ya pamoja ya jeshi

UKWELI KUHUSU MZEE MAJUTO, NA TETESI ZA KUFA